-
Kuhukumu Kahaba Mwenye Sifa MbayaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Lenye makuruhu hata kuchukiza zaidi, Yohana anaona kwamba huyo kahaba mwenyewe amelewa, amekunywa sana damu ya watumishi wa Mungu! Kwa kweli, baadaye sisi tunasoma kwamba “katika yeye ilipatikana damu ya manabii na ya watakatifu na ya wale wote ambao wamechinjwa juu ya dunia.” (Ufunuo 18:24, NW) Ni hatia ya damu kubwa mno kama nini!
26. Kuna ithibati gani ya hatia ya damu upande wa Babuloni Mkubwa?
26 Kwa muda wa karne zilizopita, milki ya ulimwengu ya dini bandia imemwaga damu nyingi kama bahari. Mathalani, katika Japani ya zamani za kale, mahekalu katika Kyoto yaligeuzwa kuwa ngome, na watawa-mashujaa-vita, wakiliitia “jina takatifu la Buddha,” walipigana vita mpaka barabara zikawa nyekundu kwa damu. Katika karne ya 20, viongozi wa kidini walipiga miguu wakiwa pamoja na majeshi ya nchi zao, na walichinjana, kukiwa na hasara ya angalau maisha milioni mia moja. Katika Oktoba 1987 Nixon aliyekuwa rais wa U.S. alisema: “Karne ya 20 imekuwa ndiyo yenye damu nyingi zaidi ya zote katika historia. Watu zaidi wameuawa katika vita vya karne hii kuliko katika vita vyote vilivyopiganwa kabla ya karne hii kuanza.” Dini za ulimwengu zimehukumiwa vibaya na Mungu kwa sababu ya ushiriki wazo katika yote haya; Yehova hukirihi “mikono ambayo inamwaga damu isiyo na hatia.” (Mithali 6:16, 17, NW) Mapema zaidi, Yohana alisikia kilio kutoka madhabahu: “Ni mpaka lini, Bwana Mwenye Enzi Kuu mtakatifu na wa kweli, wewe unajizuia usihukumu na kulipiza kisasi damu yetu juu ya wale ambao wanakaa juu ya dunia?” (Ufunuo 6:10, NW) Babuloni Mkubwa, mama ya makahaba na ya vitu vya kunyarafisha vya dunia, atahusika sana ujapo wakati wa kujibu swali hilo.
-
-
Fumbo Lenye Kutia Hofu LafumbuliwaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
1. (a) Yohana anatendaje kama itikio anapoona kahaba mkubwa na mpandwaji wake mwenye kutia hofu, na kwa nini? (b) Jamii ya Yohana inatendaje leo kama itikio, matukio yanapokunjuka katika utimizo wa njozi ya kiunabii?
TENDO-MWITIKIO la Yohana ni nini anapomwona “kahaba mkubwa” na mpandwaji wake mwenye kutia hofu? Yeye mwenyewe ajibu: “Basi, nilipoona yeye mimi nilistaajabu kwa staajabu kubwa.” (Ufunuo 17:6b, NW) Mawazo vivi hivi tu ya kibinadamu hayangeweza kutunga mwono kama huo. Hata hivyo ndio huo—mbali kule jangwani—malaya mpujufu akimpanda hayawani-mwitu wa kutisha mwenye rangi-damu-nyangavu! (Ufunuo 17:3) Jamii ya Yohana leo pia hustaajabu kwa staajabu kubwa matukio yanapokunjuka katika utimizo wa njozi ya kiunabii. Kama watu wa ulimwengu wangeweza kuiona, wao wangepaaza sauti kusema, ‘Haisadikiki!’ na watawala wa ulimwengu wangerudisha mwangwi wakisema, ‘Haifikiriki!’ Lakini njozi hiyo inakuwa uhalisi wenye kugutusha katika siku zetu. Tayari watu wa Mungu wamekuwa na ushiriki wenye kutokeza katika utimizo wa njozi hiyo, na hiyo inawahakikishia kwamba unabii huo utasonga mbele moja kwa moja mpaka upeo wao wenye kupiga butaa.
-