Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jiji Kubwa Lateketezwa
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Na yeye akalia kwa sauti imara, kusema: ‘Yeye ameanguka! Babuloni Mkubwa ameanguka.’” (Ufunuo 18:1, 2a, NW)

  • Jiji Kubwa Lateketezwa
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 5. (a) Malaika huyo anatumia nani kutoa habari ya anguko la Babuloni Mkubwa? (b) Hukumu ilipoanza juu ya wale wenye kudai kuwa “nyumba ya Mungu,” Jumuiya ya Wakristo ilikuwa hali gani?

      5 Malaika huyu mwenye mamlaka kubwa anatumia nani katika kutoa habari kama hizo zenye kushangaza mbele ya aina ya binadamu? Kwani, ni wale watu wenyewe ambao wanaachiliwa likiwa tokeo la anguko hilo, wale wapakwa-mafuta wabakio duniani, jamii ya Yohana. Kutoka 1914 mpaka 1918, hao waliteseka sana mikononi mwa Babuloni Mkubwa, lakini katika 1918 Bwana Yehova na “mjumbe wa agano [la Kiabrahamu]” wake, Yesu Kristo, alianza hukumu pamoja na “nyumba ya Mungu,” wale wenye kudai kuwa Wakristo. Hivyo Jumuiya ya Wakristo iliyoasi imani ililetwa kwenye jaribio. (Malaki 3:1; 1 Petro 4:17, NW) Hatia ya damu yayo kubwa mno iliyopata wakati wa vita ya ulimwengu ya kwanza, ushiriki wayo katika kunyanyasa mashahidi waaminifu wa Yehova, na itikadi zayo za Kibabuloni havikuisaidia katika wakati wa hukumu yayo; wala hapana sehemu nyingine yoyote ya Babuloni Mkubwa iliyostahili kibali cha Mungu.—Linga Isaya 13:1-9.

      6. Inaweza kusemwaje kwamba Babuloni Mkubwa alikuwa ameanguka kufikia 1919?

      6 Hivyo kufikia 1919 Babuloni Mkubwa alikuwa ameanguka, kufungulia njia watu wa Mungu waachiliwe na warudishwe, kana kwamba kwa siku moja, kwenye bara lao la ufanisi wa kiroho. (Isaya 66:8) Kufikia mwaka huo, Yehova Mungu na Yesu Kristo, Dario Mkubwa Zaidi na Sairasi Mkubwa Zaidi, walikuwa wameongoza mambo kwa werevu ili kwamba dini bandia isiweze tena kuwashikilia watu wa Yehova. Haingeweza tena kuwazuia wasimtumikie Yehova na kujulisha kwa wote ambao yamkini kusikia kwamba Babuloni Mkubwa aliye kama kahaba amehukumiwa uangamivu na kwamba kutetewa kwa enzi kuu ya Yehova kumekaribia karibu.—Isaya 45:1-4; Danieli 5:30, 31.

      7. (a) Ingawa Babuloni Mkubwa hakuharibiwa katika 1919, Yehova alimwonaje? (b) Babuloni Mkubwa alipoanguka katika 1919, tokeo lilikuwa nini kwa watu wa Yehova?

      7 Ni kweli, Babuloni Mkubwa hakuangamizwa katika 1919—kama vile jiji la Babuloni la kale halikuangamizwa katika 539 K.W.K. wakati lilipoanguka mikononi mwa majeshi ya Sairasi Mwajemi. Lakini kwa maoni ya Yehova, tengenezo hilo lilikuwa limeanguka. Yeye alikuwa amepata hukumu mbaya ya kimahakama, akingojea kufishwa; kwa hiyo dini bandia haingeweza kushikilia tena watu wa Yehova katika utekwa. (Linga Luka 9:59, 60.) Hao waliachiliwa wakatumikie wakiwa mtumwa mwaminifu na mwenye uangalifu wa Bwana-Mkubwa wakitoa chakula cha kiroho kwa wakati unaofaa. Wao walikuwa wamepokea hukumu ya ‘Mmefanya vema’ nao walipewa utume wajishughulishe tena na kazi ya Yehova.—Mathayo 24:45-47; 25:21, 23; Matendo 1:8, NW.

      8. Ni tukio gani ambalo mlinzi wa Isaya 21:8, 9 hupigia mbiu, na ni nani leo anayetolewa kivuli na mlinzi huyo?

      8 Mileani nyingi zilizopita Yehova alitumia manabii wengine watabiri tukio hili kubwa lenye kuanzisha muda maalumu. Isaya alisema juu ya mlinzi ambaye “aliendelea kuita kwa sauti kubwa kama simba: ‘Juu ya mnara wa lindo, O Yehova, mimi ninasimama daima mchana, na kwenye kilindio changu mimi nimewekwa mausiku yote.’” Na ni tukio gani analotambua mlinzi huyo na kupiga mbiu kwa ujasiri kama wa simba? Hili: “Yeye ameanguka! Babuloni ameanguka, na mifano yote ya kuchongwa ya miungu yake [Yehova] amevunja hadi kwenye dunia!” (Isaya 21:8, 9, NW) Mlinzi huyu anatolea kivuli vizuri jamii ya Yohana leo ambayo ni yenye kuamka kabisa, inapotumia gazeti Mnara wa Mlinzi na vichapo vingine vya kitheokrasi kuvumisha kotekote habari za kwamba Babuloni ameanguka.

      Mshuko wa Babuloni Mkubwa

      9, 10. (a) Uvutano wa dini ya Kibabuloni umepatwa na mpunguo gani tangu Vita ya Ulimwengu 1? (b) Malaika mwenye nguvu anaelezaje hali ya kuanguka ya Babuloni Mkubwa?

      9 Anguko la Babuloni wa kale katika 539 K.W.K. lilikuwa mwanzo wa mshuko mrefu ambao ulimalizikia katika ukiwa wake. Hali kadhalika, tangu vita ya kwanza ya ulimwengu, uvutano wa dini ya Kibabuloni umeshuka sana kwa kadiri ya tufe lote. Kufuata vita ya ulimwengu ya pili, ibada ya Shinto ya maliki ilikatazwa katika Japani. Katika China, serikali ya Kikomunisti hudhibiti uwekwaji rasmi na utendaji wote wa kidini. Katika Ulaya kaskazini ya Kiprotestanti, watu walio wengi wamekuwa wasiopendezwa na dini. Na hivi majuzi Kanisa Katoliki la Roma limedhoofishwa na mifarakano na kutopatana kwa ndani katika milki yalo ya tufe lote.—Linga Marko 3:24-26.

      10 Pasipo shaka miendo hii yote ni sehemu ya ‘kukauka kwa mto Eufrati’ katika kutayarishia shambulio linalokuja la kivita juu ya Babuloni Mkubwa. ‘Kukauka’ huku kunaonyeshwa, vilevile, katika tangazo la papa la Oktoba 1986 kwamba lazima kanisa ‘liwe mwomba-ombaji tena’—kwa sababu ya upungufu mkubwa mno. (Ufunuo 16:12) Hususa tangu 1919 Babuloni Mkubwa amekuwa akifichuliwa atazamwe na wote kuwa yeye ni bara-tupu la kiroho, kama malaika mwenye nguvu anavyotangaza hapa: “Na yeye amekuwa mahali pa kukaa roho waovu na mahali pa kujibanza kila pumzi isiyo safi na mahali pa kujibanza kila ndege asiye safi na mwenye kuchukiwa!” (Ufunuo 18:2b, NW) Karibuni atakuwa bara-tupu kama hilo kihalisi, akiwa ukiwa kama magofu ya Babuloni katika Iraki ya leo.—Ona pia Yeremia 50:25-28.

      11. Ni katika maana gani Babuloni Mkubwa amekuwa “mahali pa kukaa roho waovu” na ‘mahali pa kujibanza pumzi zisizo safi na pa ndege wasio safi’?

      11 Neno “roho waovu” hapa inaelekea ni mrudisho wa neno “roho waovu wenye umbo-mbuzi” (se‘i·rimʹ) linalopatikana katika elezo la Isaya kuhusu Babuloni aliyeanguka: “Na huko mizuka ya mikoa isiyo na maji kwa hakika italala chini, na nyumba zayo lazima zijawe na tai-bundi. Na huko mbuni lazima wakae, na roho waovu wenye umbo-mbuzi wenyewe wataenda wakirukaruka huko.” (Isaya 13:21, NW) Huenda isirejezee roho waovu halisi bali wanyama wakaa-jangwani wenye nywele za matimutimu ambao mwonekano wao ulifanya watazamaji wafikirie roho waovu. Katika magofu ya Babuloni Mkubwa, kuwako kitamathali kwa wanyama kama hao, pamoja na hewa tuli (“pumzi isiyo safi”) yenye sumu, na ndege wasio safi, huashiria hali yake ya kiroho iliyokufa. Yeye hatolei aina ya binadamu mataraja yoyote ya uhai.—Linga Waefeso 2:1, 2.

      12. Hali ya Babuloni Mkubwa hulandaje unabii wa Yeremia katika sura ya 50?

      12 Hali yake hulanda pia unabii wa Yeremia: “‘Kuna upanga dhidi ya Wakaldayo,’ ni tamko la Yehova, ‘na dhidi ya wakaaji wa Babuloni na dhidi ya wana-wafalme wake na dhidi ya wenye hekima wake. . . . Kuna mteketezo juu ya maji yake, na ni lazima yakaushwe kabisa. Kwa maana ni bara la mifano ya kuchongwa, na kwa sababu ya njozi zao zenye kujaa kikuli wao huendelea kutenda kikichaa. Kwa hiyo mizuka ya mikoa isiyo na maji itakaa pamoja na wanyama wenye kulia, na ndani yake yeye lazima mbuni wakae; naye hatakaliwa tena kamwe milele, wala yeye hatakaa kizazi baada ya kizazi.’” Ibada ya sanamu na kuimbwa kwa sala za kurudiwarudiwa hakuwezi kumwokoa Babuloni Mkubwa asipatwe na lipo linaloshabihi kuangushwa kwa Sodoma na Gomora na Mungu.—Yeremia 50:35-40, NW.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki