Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yesu Aja na Kitia-Moyo
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • “Yohana kwa yale makundi saba ambayo yako katika wilaya ya Esia: Na mwe na fadhili zisizostahiliwa na amani kutoka kwa ‘Yule Mmoja ambaye yuko na ambaye alikuwako na ambaye anakuja,’ na kutoka kwa zile roho saba zilizo mbele ya kiti cha ufalme chake,

  • Yesu Aja na Kitia-Moyo
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Ufunuo 1:4,

  • Yesu Aja na Kitia-Moyo
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 2. (a) Nambari “saba” inamaanisha nini? (b) Katika kipindi cha siku ya Bwana, zile jumbe kwa yale “makundi saba” zinahusu akina nani?

      2 Hapa Yohana anasema kwa “makundi saba,” na hayo yanapewa majina kwa ajili yetu baadaye katika unabii huu. Nambari hiyo, “saba,” inarudiwa mara nyingi katika Ufunuo. Inamaanisha ukamilifu, hasa kuhusiana na mambo ya Mungu na kundi lake lililopakwa mafuta. Kwa kuwa hesabu ya makundi ya watu wa Mungu ulimwenguni pote imeongezeka kufika makumi ya maelfu katika kipindi cha siku ya Bwana, sisi tunaweza kuwa na uhakika kwamba yanayosemwa kwanza kabisa kwa yale “makundi saba” ya wapakwa-mafuta yanahusu pia watu wote wa Mungu leo. (Ufunuo 1:10, NW) Ndiyo, Yohana ana ujumbe wa maana sana kwa makundi yote ya Mashahidi wa Yehova na kwa wote wanaoshirikiana nayo, kotekote usoni pa dunia hii.

      3. (a) Katika salamu ya Yohana, “fadhili zisizostahiliwa na amani” hutoka wapi? (b) Ni usemi gani wa mtume Paulo unaofanana na salamu ya Yohana?

      3 “Fadhili zisizostahiliwa na amani”—hizo ni zenye kutamanika kama nini hasa tunapothamini chanzo chazo! Yule “Mmoja” ambaye kutoka kwake zinatiririka ni Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu mwenyewe, “Mfalme wa umilele,” aishiye “kutoka wakati usio dhahiri mpaka wakati usio dhahiri.” (1 Timotheo 1:17; Zaburi 90:2, NW) Vilevile, zinazohusika hapa ni “zile roho saba,” usemi ambao unaonyesha utendaji kamili wa kani-tendaji ya Mungu, au roho takatifu, inapoleta uelewevu na baraka kwa wote wanaoupa unabii huu uangalifu. Aliye na sehemu pia ni “Yesu Kristo,” ambaye kwa habari zake Yohana aliandika baadaye hivi: “Yeye alijaa fadhili zisizostahiliwa na ukweli.” (Yohana 1:14, NW) Hivyo, salamu za Yohana zina elementi zile zile ambazo mtume Paulo alitaja katika kufunga barua yake ya pili kwa kundi la Korintho: “Fadhili zisizostahiliwa za Bwana Yesu Kristo na upendo wa Mungu na kushiriki roho takatifu ziwe pamoja nanyi nyote.” (2 Wakorintho 13:14, NW)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki