-
Mwanavita-Mfalme Asherehekea Ushindi Kwenye Har–MagedoniUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Na mimi nikaona mbingu zimefunguka, na, tazama! farasi mweupe. Na mmoja aketiye juu yake anaitwa Mwaminifu na Wa-kweli, na yeye anahukumu na kuendeleza vita katika uadilifu.
-
-
Mwanavita-Mfalme Asherehekea Ushindi Kwenye Har–MagedoniUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
5, 6. Ni nini kinachoashiriwa na (a) “farasi mweupe”? (b) jina “Mwaminifu na Wa-kweli”? (c) macho kama “mwali wa moto”? (d) “mataji mengi”?
5 Kama katika njozi ya mapema zaidi ya wapanda-farasi wanne, huyu “farasi mweupe” ni ufananisho unaofaa wa vita yenye uadilifu. (Ufunuo 6:2, NW) Na ni yupi wa wana wa Mungu ambaye angekuwa mwadilifu zaidi ya Mwanavita huyu? Akiwa “anaitwa Mwaminifu na Wa-kweli,” lazima yeye awe “shahidi mwaminifu na wa kweli,” Yesu Kristo. (Ufunuo 3:14, NW) Yeye hufanya vita ili kutekeleza hukumu za uadilifu za Yehova. Hivyo, yeye anatenda akiwa katika cheo chake cha Hakimu aliyewekwa rasmi na Yehova, cha kuwa “Mungu Mwenye Nguvu.” (Isaya 9:6, NW)
-