-
UfufuoKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
(Wale wafu wengine hawakuwa hai mpaka ile miaka elfu ilipokwisha.) Huo ndio ufufuo wa kwanza.
-
-
UfufuoKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Mabano yanatumiwa katika NW na BHN ili kumsaidia msomaji aone uhusiano kati ya maneno yaliyo baada na kabla ya mabano. Kama ilivyosemwa waziwazi, wale wanaopata ufufuo wa kwanza si “wale wafu wengine.” Ufufuo huo ni wa wale wanaotawala pamoja na Kristo kwa miaka elfu. Je, hilo linamaanisha kwamba hakuna wanadamu wengine watakaoishi wakati wa miaka elfu isipokuwa wale wanaotawala mbinguni pamoja na Yesu? Sivyo; kwa sababu, ikiwa ingekuwa hivyo, ingemaanisha kwamba hakungekuwa na mtu ambaye wangemtumikia wakiwa makuhani, na milki yao ingekuwa dunia isiyo na kitu.
Basi, “wale wafu wengine” ni nani? Ni wale wanadamu wengine wote waliokufa kwa sababu ya dhambi ya Adamu na wale ambao, wajapokuwa waokokaji wa dhiki kuu au wale ambao huenda wakazaliwa wakati wa ile Miaka Elfu, wanahitaji kuondolewa matokeo yenye kuleta kifo ya dhambi hiyo.—Linganisha na Waefeso 2:1.
Ni katika maana gani ‘hawawi hai’ mpaka mwisho wa ile miaka elfu? Hilo halimaanishi ufufuo wao. Huku ‘kuwa hai’ kunatia ndani mengi kuliko kuwako tu wakiwa wanadamu. Humaanisha kufikia kuwa wanadamu wakamilifu, wasio na madhara yoyote ya dhambi ya Adamu. Ona kwamba mtajo wa jambo hilo katika mstari wa 5 hutukia mara baada ya mstari unaotangulia kusema kwamba wale watakaokuwa mbinguni ‘walikuwa hai.’ Kwa hao, inamaanisha kwamba watakuwa na uzima usio na dhambi yoyote ya Adamu; hata wanapewa pendeleo la pekee la uzima usioweza kufa. (1 Kor. 15:54) Basi, kwa habari ya “wale wafu wengine,” lazima imaanishe uzima mkamilifu wa kibinadamu.
-