-
Kuponda Kichwa cha NyokaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Na wao walisonga mbele juu ya upana wa dunia na kuzingira kambi ya watakatifu na jiji lenye kupendwa.”—Ufunuo 20:7-9a, NW.
-
-
Kuponda Kichwa cha NyokaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
24. (a) Ni nini lililo “jiji lenye kupendwa” nalo linaweza kuzingirwaje? (b) Ni nini kinachowakilishwa na “kambi ya watakatifu”?
24 “Jiji lenye kupendwa” lazima liwe jiji ambalo Yesu Kristo aliyetukuzwa anasema juu yalo kwa wafuasi wake kwenye Ufunuo 3:12 na ambalo yeye anaita “jiji la Mungu wangu, Yerusalemu jipya ambalo hushuka kutoka katika mbingu kutoka kwa Mungu wangu.” Kwa kuwa hili ni tengenezo la kimbingu, kani hizo za kidunia zingewezaje ‘kulizingira’? Ni kwa vile wao huzingira “kambi ya watakatifu.” Kambi huwa nje ya jiji; kwa hiyo, “kambi ya watakatifu” lazima iwakilishe wale walio duniani nje ya mahali pa kimbingu pa Yerusalemu Jipya ambao kwa ushikamanifu hutegemeza mpango wa Yehova wa kiserikali. Wakati waasi hao walio chini ya Shetani wanaposhambulia wale waaminifu, Bwana Yesu huona hilo kuwa ni shambulio juu ya yeye. (Mathayo 25:40, 45) “Yale mataifa” yatajaribu kufutilia mbali yote ambayo Yerusalemu Jipya la kimbingu limetimiza katika kufanya dunia paradiso. Hivyo kwa kushambulia “kambi ya watakatifu,” wao wanashambulia pia “jiji lenye kupendwa.”
Ziwa la Moto na Salfa
25. Yohana anaelezaje tokeo la shambulio la waasi juu ya “kambi ya watakatifu,” na litamaanisha nini kwa Shetani?
25 Je! jitihada hii ya mwisho kabisa ya Shetani itafaulu? Hakika sivyo—kama vile shambulio ambalo Gogu wa Magogu anatazamiwa kufanya juu ya Israeli wa kiroho katika siku yetu halitafaulu! (Ezekieli 38:18-23) Yohana anaeleza waziwazi tokeo: “Lakini moto ulikuja chini kutoka katika mbingu na ukameza wao.
-