Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Siku ya Hukumu ya Mungu—Matokeo Yayo Yenye Shangwe!
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • “Na mimi nikaona wafu, wakubwa na wadogo, wakisimama mbele ya kiti cha ufalme na hati-kunjo zilifunguliwa.” (Ufunuo 20:12a, NW) “Wakubwa na wadogo” hutia ndani walio mashuhuri pamoja na wasio mashuhuri sana wa wanadamu ambao wameishi na wakafa kwenye dunia hii wakati wa miaka 6,000 iliyopita. Katika Gospeli ambayo Yohana aliandika muda mfupi baada ya Ufunuo, Yesu alisema kwa habari ya Baba yake: “Naye akampa [Yesu] amri ya kufanya hukumu kwa sababu ni Mwana wa Adamu. Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake. Nao watatoka.” (Yohana 5:27-29) Ni mradi mkubwa ajabu kama nini—kutangua vifo na makaburi ya muda wote wa historia! Hapana shaka hayo mamilioni yasiyohesabika yaliyo katika kumbukumbu la Mungu watatokezwa hatua kwa hatua hivi kwamba umati mkubwa—ambao ni wachache sana kwa kulinganisha—utaweza kushughulikia matatizo ambayo huenda yatazuka kwa sababu huenda mwanzoni wafufuliwa wakaelekea kufuata mtindo wao wa maisha ya kale, pamoja na udhaifu wa mnofu wao na mielekeo.

      Nani Wanainuliwa na Kuhukumiwa?

      7, 8. (a) Ni hati-kunjo gani inayofunguliwa, na ni jambo gani linalotukia baada ya hapo? (b) Ni kwa akina nani hakutakuwa na ufufuo?

      7 Yohana anaongeza: “Lakini hati-kunjo nyingine ikafunguliwa; ndiyo hati-kunjo ya uhai. Na wafu walihukumiwa kutoka kwa vile vitu vilivyoandikwa katika hati-kunjo kulingana na matendo yao.

  • Siku ya Hukumu ya Mungu—Matokeo Yayo Yenye Shangwe!
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Ufunuo 20:12b,

  • Siku ya Hukumu ya Mungu—Matokeo Yayo Yenye Shangwe!
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Hati-Kunjo ya Uhai

      11. (a) “Hati-kunjo ya uhai” ni nini, na ni majina ya nani yaliyorekodiwa katika hati-kunjo hii? (b) Ni kwa nini hati-kunjo ya uhai itafunguliwa wakati wa Utawala wa Miaka Elfu?

      11 Yohana husema juu ya “hati-kunjo ya uhai.” Hayo ni maandishi ya wale walio katika mstari wa kupokea uhai wa milele kutoka kwa Yehova. Majina ya ndugu wapakwa-mafuta wa Yesu, ya umati mkubwa, na ya watu waaminifu wa kale, kama vile Musa, yameandikwa katika hati-kunjo hii. (Kutoka 32:32, 33; Danieli 12:1; Ufunuo 3:5, NW) Bado kufikia hapa, hakuna hata mmoja wa wale “wasio waadilifu” waliofufuliwa aliye na jina lake limeandikwa katika hati-kunjo ya uhai. Kwa hiyo hati-kunjo ya uhai itafunguliwa wakati wa Utawala wa Miaka Elfu kuruhusu kuandikwa kwa majina ya wengine ambao wanakuja kustahili. Wale ambao majina yao hayapati kuandikwa katika hati-kunjo au kitabu, ya uhai ‘wanavurumishwa ndani ya ziwa la moto.’—Ufunuo 20:15, NW; linga Waebrania 3:19.

      12. Ni nini kitakachoamua kama mtu ataandikisha jina lake katika hati-kunjo ya uhai iliyofunguliwa, na Hakimu mwekwa wa Yehova aliwekaje kielelezo?

      12 Basi, ni nini kitakachoamua kama mtu anapata kuandikisha jina lake katika hati-kunjo ya uhai iliyofunguliwa wakati huo? Sababisho kuu litakuwa lile lile kama lilivyokuwa katika siku ya Adamu na Hawa: utii kwa Yehova. Kama vile mtume Yohana alivyoandikia Wakristo wenzake wapendwa: “Ulimwengu unapitilia mbali na ndivyo na tamaa yao, lakini yeye ambaye hufanya mapenzi ya Mungu hubaki milele.” (1 Yohana 2:4-7, 17, NW) Kwa habari ya utii, Hakimu mwekwa wa Yehova aliweka kielelezo: “Ingawa [Yesu] alikuwa Mwana, yeye alijifunza kutii kutokana na vitu ambavyo yeye aliteseka; na baada ya yeye kuwa amefanywa mkamilifu, yeye alipata kuwa mwenye daraka la wokovu wa milele kwa wale wote wanaotii yeye.”—Waebrania 5:8, 9, NW.

      Kufungua Hati-Kunjo Nyingine

      13. Ni lazima wafufuliwa waonyesheje utii wao, na ni kanuni gani ambazo lazima wafuate?

      13 Ni lazima hawa wafufuliwa waonyesheje utii wao? Yesu mwenyewe alielekeza kwenye amri mbili kubwa, akisema: “Ya kwanza ni, ‘Sikia O Israeli, Yehova Mungu wetu ni Yehova mmoja, na wewe lazima upende Yehova Mungu wako kwa moyo mzima wote na kwa nafsi nzima yote na kwa akili nzima zote na kwa uthabiti mzima wote.’ Ya pili ni hii, ‘Lazima wewe upende jirani yako kama wewe mwenyewe.’” (Marko 12:29-31, NW) Pia kuna kanuni za Yehova zilizoimarishwa vizuri ambazo lazima wafuate, kama vile kukataa katakata kuiba, kusema uwongo, kuua kimakusudi, na utovu wa adili.—1 Timotheo 1:8-11; Ufunuo 21:8.

      14. Ni hati-kunjo gani nyingine zinazofunguliwa, na ni mambo gani yaliyomo?

      14 Hata hivyo, ndipo Yohana ametoka tu kutaja hati-kunjo nyingine ambazo zitafunguliwa wakati wa Utawala wa Mileani. (Ufunuo 20:12) Hizi zitakuwa nini? Nyakati fulani, Yehova ametoa maagizo yaliyo waziwazi katika hali maalumu. Mathalani, katika siku ya Musa yeye aliandaa mfululizo wa sheria zenye mambo mengi-mengi ambazo zilimaanisha uhai kwa Waisraeli ikiwa wangetii. (Kumbukumbu 4:40; 32:45-47) Wakati wa karne ya kwanza, maagizo mapya yalitolewa kusaidia waaminifu kufuata kanuni za Yehova chini ya mfumo wa mambo wa Kikristo. (Mathayo 28:19, 20; Yohana 13:34; 15:9, 10) Sasa Yohana anaripoti kwamba wafu ‘watahukumiwa kutoka kwa vile vitu vilivyoandikwa katika hati-kunjo kulingana na matendo yao.’ Kwa wazi, basi, kufunguliwa kwa hati-kunjo hizi kutatangaza matakwa ya Yehova yenye mambo mengi-mengi kwa ajili ya aina ya binadamu wakati wa miaka elfu. Kwa kutumia katika maisha yao virekebi na amri za hati-kunjo hizo, wanadamu watiifu wataweza kurefusha siku zao, wakifikia mwishowe uhai wa milele.

      15. Ni kampeni ya kielimu ya aina gani itakayohitajiwa wakati wa ufufuo, na yaelekea ufufuo utaendeleaje?

      15 Ni kampeni iliyopanuka kama nini ya elimu ya kitheokrasi itakayohitajiwa! Katika 2005 Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote walikuwa wakiongoza, kwa wastani, mafunzo ya Biblia 6,061,534 katika mahali pa namna namna. Lakini wakati wa ufufuo, mamilioni yasiyohesabika ya mafunzo, msingi wayo ukiwa Biblia na hati-kunjo mpya, yataongozwa bila shaka! Watu wote wa Mungu watahitaji kuwa walimu na kujitahidi wenyewe. Wafufuliwa, kadiri waendeleavyo, pasipo shaka watashiriki programu hii iliyo kubwa mno ya kufundisha. Yaelekea, ufufuo utaendelea katika njia ya kwamba wale walio hai watapata kuwa na shangwe ya kukaribisha na kufundisha washiriki wa jamaa wa zamani na watu waliojuana nao, ambao, nao kwa zamu yao, watapata kukaribisha na kufundisha wengine. (Linga 1 Wakorintho 15:19-28, 58.) Wale Mashahidi wa Yehova zaidi ya milioni sita ambao ni watendaji katika kueneza ukweli leo wanaweka msingi mwema kwa ajili ya mapendeleo wanayotumainia kupata katika wakati wa ufufuo.—Isaya 50:4; 54:13.

      16. (a) Ni majina ya nani ambayo hayataandikwa katika hati-kunjo, au kitabu, ya uhai? (b) Ni nani wale ambao ufufuo wao utathibitika kuwa “wa uhai”?

      16 Kwa habari ya ufufuo wa kidunia, Yesu alisema kwamba ‘wale waliofanya mema hutoka na kuja kwenye ufufuo wa uhai, wale waliozoea vitu vibaya sana kwenye ufufuo wa hukumu.’ Hapa “uhai” na “hukumu” hutofautiana, kuonyesha kwamba wale wafufuliwa ambao ‘huzoea vitu vibaya sana’ baada ya kufundishwa katika Maandiko na hati-kunjo zilizovuviwa huhukumiwa kuwa hawastahili uhai. Majina yao hayataandikwa katika hati-kunjo au kitabu, ya uhai. (Yohana 5:29, NW) Inaweza kuwa hivyo pia kwa wowote ambao hapo kwanza walifuata mwendo wa uaminifu lakini ambao, kwa sababu fulani, wanakengeuka katika wakati wa Utawala wa Miaka Elfu. Majina yanaweza kufutwa. (Kutoka 32:32, 33) Kwa upande mwingine, wale ambao kwa kutii hufuata vitu vilivyoandikwa katika hati-kunjo watatunza majina yao katika rekodi iliyoandikwa, hati-kunjo ya uhai, na kuendelea kuishi. Kwa wao, ufufuo utakuwa umethibitika kuwa “wa uhai.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki