-
Jiji Lenye Uzuri wa Kung’aaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Na mimi sikuona hekalu ndani yalo, kwa maana Yehova Mungu Mweza Yote ndiye hekalu lalo, pia Mwana-Kondoo.
-
-
Jiji Lenye Uzuri wa Kung’aaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Kwa kweli, hakuna haja ya kujenga hekalu halisi hapa. Hekalu la kale la Kiyahudi lilikuwa kigezo, na uhalisi wa kigezo hicho, hekalu kubwa la kiroho, umekuwako tangu Yehova alipompaka mafuta Yesu awe Kuhani Mkuu katika 29 W.K. (Mathayo 3:16, 17; Waebrania 9:11, 12, 23, 24) Pia hekalu hutangulia kudokezea jamii ya kikuhani ikitoa dhabihu kwa Yehova kwa ajili ya watu. Lakini wale wote ambao wanajumlika kuwa Yerusalemu Jipya ni makuhani. (Ufunuo 20:6) Na dhabihu kubwa, uhai mkamilifu wa kibinadamu wa Yesu, umekwisha tolewa mara moja kwa wakati wote. (Waebrania 9:27, 28) Na zaidi, Yehova anafikilika kibinafsi na yeyote anayeishi katika jiji.
-