-
Iweni Wasomaji Wenye Furaha wa Kitabu cha UfunuoMnara wa Mlinzi—1999 | Desemba 1
-
-
“Maneno haya ni ya uaminifu na ya kweli; ndiyo, Yehova Mungu wa semi zilizopuliziwa za manabii alimtuma malaika wake kuonyesha watumwa wake mambo ambayo lazima yatukie upesi
-
-
Iweni Wasomaji Wenye Furaha wa Kitabu cha UfunuoMnara wa Mlinzi—1999 | Desemba 1
-
-
17. (a) Andiko la Ufunuo 22:6 latuhakikishia nini? (b) Ni lazima tuwe macho kuepuka nini?
17 Wasomaji wenye furaha wa Ufunuo watakumbuka kwamba maneno yanayofanana na haya yanatajwa mwanzoni mwa “hati-kunjo.” (Ufunuo 1:1, 3) Maneno haya yatuhakikishia kwamba “mambo” yote yaliyotabiriwa katika kitabu hiki cha mwisho cha Biblia ‘yatatukia upesi.’ Twaishi katika kipindi cha mwisho kabisa hivi kwamba mambo yanayotuhusu ambayo yalitabiriwa katika Ufunuo kwa hakika ni lazima yatukie upesi, yakifuatana haraka-haraka. Kwa hiyo uthabiti wowote ule uonekanao katika mfumo wa Shetani haupaswi kutufanya tulale usingizi. Msomaji makini atakumbuka maonyo yaliyotolewa katika ujumbe ambao ulipelekwa kwenye makutaniko saba ya Asia naye ataepuka mitego ya kufuatia vitu vya kimwili, ibada ya sanamu, ukosefu wa adili, uvuguvugu, na uasi-imani wenye mafarakano.
-