-
Je! Jina Lako Limo Katika Kitabu cha Uhai?Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Hata hivyo, wewe una majina machache katika Sardisi ambayo hayakuchafua mavazi yao ya nje, nao watatembea pamoja na mimi katika meupe, kwa sababu wao wanastahiki.
-
-
Je! Jina Lako Limo Katika Kitabu cha Uhai?Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Kwa sababu ya uzembe upande wa baraza la wazee, kundi kwa ujumla huenda likaingia ndani ya usingizi wa kiroho. Hata hivyo, baadhi ya watu mmoja mmoja humo huenda wakajitahidi kishujaa kutunza utambulisho wao wa Kikristo ukiwa safi na bila kutiwa madoa na hivyo waendelee kuwa na jina zuri pamoja na Yehova.—Mithali 22:1.
11, 12. (a) Hata katika pindi ya ule uasi-imani mkubwa, ni lazima wengine wawe walikuwaje kama yale “majina machache” yenye uaminifu katika Sardisi? (b) Ni kitulizo gani kilichowajia Wakristo wa mfano wa ngano wakati wa siku ya Bwana?
11 Ndiyo, hayo “mavazi ya nje” yanarejeza kwenye utambulisho wa uadilifu wa mtu akiwa Mkristo. (Linga Ufunuo 16:15; 19:8.) Ni lazima Yesu achangamke moyo kuona kwamba, kujapokuwa utepetevu wa idadi iliyo kubwa, “majina machache,” Wakristo wapakwa-mafuta wachache katika Sardisi, bado wanafaulu kuendeleza utambulisho huu. Vivyo hivyo, wakati waliodai kuwa Wakristo walipovama katika Babuloni Mkubwa, ile milki ya ulimwengu ya dini bandia, wakati wa zile karne ndefu za ule uasi-imani mkubwa, ni lazima kuwe sikuzote kulikuwako watu wachache mmoja mmoja waliojaribu kufanya mapenzi ya Mungu, ijapokuwa vipingamizi vikubwa. Hawa walikuwa waadilifu kama ngano iliyofichwa kati ya mvuvumuko wa magugu ya kifarakano.—Ufunuo 17:3-6; Mathayo 13:24-29.
12 Yesu aliahidi kwamba yeye angekuwa pamoja na Wakristo hao mfano wa ngano “sikuzote mpaka umalizio wa mfumo wa mambo.” Yeye anajua wao ni akina nani na ni jina gani zuri walilojifanyia wenyewe. (Mathayo 28:20, NW; Mhubiri 7:1) Ebu wazia shangilio la hao waaminifu ‘wachache’ ambao walikuwa wangali hai mwanzoni mwa siku ya Bwana! Mwishowe walitenganishwa na Jumuiya ya Wakristo iliyokufa kiroho nao walikusanywa wakaingizwa ndani ya kundi lenye uadilifu linalofanana zaidi na lile kundi katika Smirna.—Mathayo 13:40-43.
13. Ni baraka gani zilizo akibani kwa Wakristo wapakwa-mafuta ambao ‘hawachafui mavazi yao ya nje’?
13 Wale katika Sardisi ambao ni waaminifu mpaka mwisho na hawachafui utambulisho wao wa Kikristo wanafikia utimizo wa tumaini zuri ajabu. Baada ya kusimamishwa kwa Ufalme wa Kimesiya katika 1914, wanafufuliwa kwenye uhai wa kiroho na wakiwa washindi hupambwa mavazi meupe ya nje yakiwa ufananisho wa uadilifu wao usio na kasoro, wala waa. Wakiwa wamekwisha tembea katika ile njia yenye kusonga iongozayo kwenye uhai, watafurahia thawabu ya milele.—Mathayo 7:14; Ona pia Ufunuo 6:9-11.
-