Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Uzuri Mwingi Mno wa Kiti cha Ufalme cha Yehova cha Kimbingu
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Meme, Sauti, na Ngurumo

      12. Ni nini kinachofuata kuonwa na kusikiwa na Yohana, na “meme na sauti na ngurumo” huleta nini akilini?

      12 Ni nini kinachofuata kuonwa na kusikiwa na Yohana? “Na katika kiti cha ufalme zinatoka meme na sauti na ngurumo.” (Ufunuo 4:5a, NW) Lo! jinsi inavyokumbusha madhihirisho mengine yenye kutia hofu ya uwezo wa kimbingu wa Yehova! Mathalani, wakati Yehova ‘aliposhuka’ juu ya Mlima Sinai, Musa aliripoti hivi: “Katika siku ya tatu wakati ilipokuwa asubuhi, ikawa kwamba ngurumo na meme zikaanza kutukia, na wingu zito juu ya mlima na sauti kubwa sana ya pembe. . . . Wakati sauti ya pembe iliendelea kuwa kubwa zaidi na zaidi, Musa akaanza kunena, na Mungu wa kweli akaanza kujibu yeye kwa sauti.”—Kutoka 19:16-19, NW.

      13. Ni nini kinachoonyeshwa na picha ya meme zinazotoka katika kiti cha ufalme cha Yehova?

      13 Katika kipindi cha siku ya Bwana, Yehova hufanya nguvu na kuwapo kwake vidhihirike kwa njia yenye ukwezo mkubwa mno. La, si kwa umeme halisi, kwa kuwa Yohana anaona ishara. Basi, meme hizo zinawakilisha nini? Basi, mimeto ya umeme inaweza kunurisha, lakini inaweza pia kumpiga mtu mpaka kufa. Kwa hiyo, meme hizi zinazotoka kwenye kiti cha ufalme cha Yehova hufananisha kwa kufaa ile mimeto ya nuru ya elimu ambayo yeye amekuwa akiwapa watu wake kwa kuendelea na, hata la maana zaidi, jumbe zake za hukumu zenye moto.—Linga Zaburi 18:14; 144:5, 6; Mathayo 4:14-17; 24:27.

      14. Sauti zimevumaje leo?

      14 Namna gani zile sauti? Wakati wa kushuka kwa Yehova juu ya Mlima Sinai, sauti ilinena kwa Musa. (Kutoka 19:19) Sauti kutoka mbinguni zilitoa nyingi za zile amri na mbiu katika kitabu cha Ufunuo. (Ufunuo 4:1; 10:4, 8; 11:12; 12:10; 14:13; 16:1, 17; 18:4; 19:5; 21:3) Leo, Yehova ametoa pia amri na mbiu kwa watu wake, akimulikia kuelewa kwao unabii na kanuni za Biblia. Habari yenye kutoa nuru ya elimu mara nyingi imejulishwa kwenye mikusanyiko ya kimataifa, kisha, mbiu ya kweli hizo za Biblia imepigwa ulimwenguni pote. Mtume Paulo alisema hivi juu ya wahubiri waaminifu wa habari njema: “Kwani, kwa hakika, ‘katika dunia yote mvumo wao ulitoka ukaenda, na kwenye ncha za dunia inayokaliwa matamko yao.’”—Warumi 10:18, NW.

      15. Ni ngurumo gani ambazo zimetoka katika kiti cha ufalme katika sehemu hii ya siku ya Bwana?

      15 Kwa kawaida ngurumo hufuatana na umeme. Daudi alirejezea ngurumo halisi kuwa “sauti ya Yehova.” (Zaburi 29:3, 4, NW) Wakati Yehova alipopigania Daudi dhidi ya adui zake, ngurumo ilisemekana kuwa ilitoka kwa Yeye. (2 Samweli 22:14; Zaburi 18:13) Elihu alimwambia Ayubu kwamba sauti ya Yehova ilivuma kama ngurumo, Yeye anapofanya “vitu vikubwa ambavyo sisi hatuwezi kujua.” (Ayubu 37:4, 5, NW) Wakati wa sehemu hii ya siku ya Bwana, Yehova ‘amenguruma,’ akionya juu ya matendo makubwa ambayo atafanya dhidi ya adui zake. Hii milio ya ufananisho ya ngurumo imetoa mwangwi na ikatoa mwangwi tena na tena katika dunia yote. Wewe ni mwenye furaha ikiwa umesikiliza matangazo haya yenye ngurumo na unatumia ulimi wako katika kuongezea ukubwa wayo!—Isaya 50:4, 5; 61:1, 2.

      Taa za Moto na Bahari ya Kioo

      16. Ni jambo gani linalomaanishwa na zile “taa saba za moto”?

      16 Yohana anaona nini zaidi? Hiki: “Na kuna taa saba za moto zikiwaka mbele ya kiti cha ufalme, na hizi humaanisha roho saba za Mungu. Na mbele ya kiti cha ufalme kuna, kana kwamba, ni bahari ya kioo kama fuwele.” (Ufunuo 4:5b, 6a, NW) Yohana mwenyewe anatuambia maana ya hizo taa saba: “Hizi humaanisha roho saba za Mungu.” Nambari saba hufananisha utimilifu wa kimungu; kwa hiyo taa saba lazima ziwakilishe ule ujazo wa kani ya roho takatifu yenye kutoa nuru ya elimu. Jinsi ile jamii ya Yohana ilivyo yenye kushukuru leo kwa vile imeaminishwa hii nuru ya elimu, pamoja na lile daraka la kuipitisha kwenye vikundi vya watu wa dunia wenye njaa ya kiroho! Jinsi tunavyoterema kwamba kila mwaka mamilioni ya nakala za gazeti Mnara wa Mlinzi yanaendelea kuangaza nuru katika lugha zipatazo 150!—Zaburi 43:3.

  • Uzuri Mwingi Mno wa Kiti cha Ufalme cha Yehova cha Kimbingu
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • [Picha ya ukurasa mzima katika ukurasa wa 78]

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki