Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Abrahamu—Kielelezo cha Imani
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Agosti 15
    • Ng’ambo ya Eufrati

      13. Abramu alivuka Mto Eufrati lini, na kuvuka huko kulimaanisha nini?

      13 Ilimbidi Abramu asafiri tena. Aliondoka Harani na kusafiri umbali upatao kilometa 90 kuelekea magharibi. Huenda ikawa kwamba Abramu alikaa kwa muda katika eneo fulani kwenye Eufrati, ng’ambo ya kituo cha kale cha biashara cha Karkemishi. Kituo hicho kilikuwa muhimu kwa misafara iliyovuka kwenda ng’ambo ya pili.b Msafara wa Abramu ulivuka mto huo lini? Biblia inaonyesha kwamba ulivuka miaka 430 kabla ya kule Kutoka kwa Wayahudi nchini Misri mwezi wa Nisani 14, 1513 K.W.K. Andiko la Kutoka 12:41 lasema: “Ilikuwa mwisho wa miaka hiyo mia nne na thelathini, ilikuwa siku ile ile, ya kwamba majeshi yote ya BWANA yalitoka nchi ya Misri.” (Italiki ni zetu.) Basi inaelekea kwamba lile agano la Kiabrahamu lilianza kufanya kazi Nisani 14, 1943 K.W.K., wakati ambapo kwa utii Abramu alivuka Eufrati.

  • Abrahamu—Kielelezo cha Imani
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Agosti 15
    • b Karne kadhaa baadaye, Mfalme Ashurnasirpal wa Pili wa Ashuru alitumia vyelezo kuvuka Eufrati karibu na Karkemishi. Biblia haisemi iwapo Abramu na msafara wake walitumia vyelezo au hawakuvitumia kuvuka mto huo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki