Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Luka—Mfanyakazi Mwenzi Mpendwa
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Novemba 15
    • Mwandikaji na Mmishonari

      Injili ya Luka na pia kitabu cha Matendo ya Mitume kimeelekezwa kwa Theofilo, na hilo linaonyesha kwamba vitabu hivyo viwili vilivyoongozwa na roho viliandikwa na Luka. (Luka 1:3; Matendo 1:1)

  • Luka—Mfanyakazi Mwenzi Mpendwa
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Novemba 15
    • Ingawa Luka hatajwi katika kitabu cha Matendo, anajihusisha katika masimulizi fulani na hivyo anaonyesha kwamba alihusika katika matukio hayo. Luka anapozungumzia matukio katika safari ya Paulo na waandamani wake kupitia Asia Ndogo, anasema hivi: “Wakapita Misia na kushuka mpaka Troa.” Wakiwa Troa Paulo alipata maono ya mwanamume Mmakedonia ambaye alisihi hivi: “Vuka uingie Makedonia utusaidie.” Luka anaongezea: “Basi mara tu alipokuwa amekwisha kuona maono hayo, tukajaribu kuingia Makedonia.” (Matendo 16:8-10) Kwa kuwa mwanzoni alisema “wakapita” na baadaye anasema “tukajaribu,” inaelekea Luka alijiunga na Paulo na wenzake huko Troa. Kisha, Luka anaeleza kuhusu kazi ya kuhubiri huko Filipi kwa njia inayoonyesha kwamba alishiriki kazi hiyo. “Siku ya sabato,” Luka anaandika, “tukatoka nje ya lango kando ya mto, ambapo tulikuwa tukifikiri kwamba palikuwa na mahali pa sala; nasi tukaketi na kuanza kusema na wanawake waliokuwa wamekusanyika.” Matokeo yalikuwa kwamba Lidia na watu wote wa nyumbani mwake walikubali habari njema na kubatizwa.—Matendo 16:11-15.

      Upinzani ulitokea huko Filipi, ambako Paulo alimponya kijakazi aliyekuwa akibashiri kwa uwezo wa “roho mwovu wa uaguzi.” Mabwana wake walipoona kwamba chanzo chao cha mapato kimeondolewa, waliwashika Paulo na Sila. Baadaye Paulo na Sila walipigwa na kutupwa gerezani. Inaelekea kwamba Luka hakukamatwa, kwa sababu hajihusishi anapoeleza mambo yaliyowapata wenzake. Walipoachiliwa, ‘Paulo na Sila waliwatia moyo akina ndugu kisha wakaondoka.’ Baadaye Luka anaanza tena kujihusisha katika masimulizi hayo wakati Paulo anaporudi Filipi. (Matendo 16:16-40; 20:5, 6) Huenda Luka alibaki Filipi ili kusimamia kazi katika eneo hilo.

      Kukusanya Habari

      Luka alipata jinsi gani habari alizoandika katika Injili yake na katika kitabu cha Matendo? Sehemu za kitabu cha Matendo ambazo Luka anajihusisha katika masimulizi, zinaonyesha kwamba Luka alisafiri na Paulo kutoka Filipi kwenda Yerusalemu, ambako mtume huyo alikamatwa tena. Wakiwa njiani, Paulo na wenzake walikaa na Filipo, yule mweneza-injili huko Kaisaria. (Matendo 20:6; 21:1-17) Luka angeweza kupata habari kuhusu kazi ya mapema ya umishonari huko Samaria kutoka kwa Filipo mwenyewe, ambaye aliongoza kazi ya kuhubiri katika eneo hilo. (Matendo 8:4-25)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki