-
Kwa Nini Niepuke Ponografia?Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
-
-
Kutazama ponografia kunaweza kuwa zoea lenye madhara ya kudumu. Kwa mfano, mfikirie Jeff ambaye hata baada ya miaka 14 kupita tangu alipoacha kutazama ponografia, anasema: “Mimi hupambana kila siku. Ingawa si kama zamani, bado mimi huwa na hamu ya kuitazama. Picha hizo zingali akilini. Laiti singeanza zoea hilo. Mwanzoni sikuona ubaya wowote. Lakini sasa ninajua. Ponografia inadhuru, ni potovu, na inawashushia heshima wote wanaohusika. Hata wale wanaoitetea waseme nini, ponografia haina faida yoyote.”
-
-
Kwa Nini Niepuke Ponografia?Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
-
-
Ikiwa Tayari Una Zoea Hilo
Kuona ponografia bila kukusudia ni tofauti kabisa na kuitazama kimakusudi. Namna gani ikiwa limeanza kuwa zoea? Usidanganyike, si rahisi kuacha zoea hilo. Tuseme mikono yako imefungwa pamoja kwa uzi mmoja. Huenda ungeweza kujinasua kwa urahisi kwa kuukata uzi huo. Lakini namna gani ikiwa uzi huo ungezungushwa mikononi mwako mara nyingi? Ingekuwa vigumu kujinasua. Ndivyo ilivyo na watu ambao wana mazoea ya kutazama ponografia. Kadiri wanavyoitazama, ndivyo wanavyozidi kunaswa. Ikiwa tayari una mazoea hayo, unaweza kufanya nini?
Tambua mtego wa ponografia. Shetani hutumia ponografia kuvunjia heshima kitu ambacho Yehova aliumba kiheshimike. Kuwa na maoni hayo kutakusaidia ‘kuchukia yaliyo mabaya.’—Zaburi 97:10.
Fikiria madhara. Ponografia huharibu ndoa. Inawashushia heshima wahusika. Inamshushia heshima mtu anayeitazama. Ndiyo sababu Biblia inasema: “Mtu mwerevu ni yule ambaye ameona msiba na kujificha.” (Methali 22:3) Andika hapa chini mfano mmoja wa msiba unaoweza kukupata ukiwa na zoea la kutazama ponografia.
․․․․․
Jiwekee azimio. Mwanamume mwaminifu Ayubu alisema: “Nimejifunga rasmi mimi mwenyewe, macho yangu yasimtazame msichana kwa tamaa.” (Ayubu 31:1, BHN) Wewe pia unaweza ‘kujifunga rasmi’ kwa kufanya yafuatayo:
Sitatumia Intaneti kamwe nikiwa peke yangu chumbani.
Nitafunga mara moja kituo chochote kinachoonyesha mambo ya ngono.
Nitazungumza na rafiki mkomavu iwapo nitatumbukia tena katika zoea hilo.
Kuna jambo au mambo mengine yanayoweza kukusaidia kushinda tatizo la kutazama ponografia? Yaandike hapa chini.
․․․․․
Sali kuhusu jambo hilo. Mtunga-zaburi alisali hivi kwa Yehova: “Uyafanye macho yangu yapite ili yasione jambo lisilofaa.” (Zaburi 119:37) Yehova Mungu anataka ufaulu, naye anaweza kukupa nguvu za kufanya yaliyo sawa!—Wafilipi 4:13.
Zungumza na mtu. Mara nyingi kuchagua mtu unayeweza kumfunulia moyo wako husaidia sana kushinda zoea hilo. (Methali 17:17) Andika hapa chini jina la mtu mkomavu ambaye unaona ni rahisi kumweleza jambo hilo.
-
-
Kwa Nini Niepuke Ponografia?Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
-
-
[Blabu katika ukurasa wa 278]
‘‘Kabla ya kujifunza Biblia, nilikuwa nimetumia kwa wingi karibu dawa zote za kulevya. Lakini kati ya mazoea yangu yote, ilikuwa vigumu zaidi kuacha kutazama ponografia. Yehova amenisaidia kupambana na tatizo hilo.’’—Jeff
-