Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Madhara Yanayosababishwa na Ponografia
    Amkeni!—2003 | Julai 22
    • Kuacha Zoea la Kutazama Ponografia

      Vipi ikiwa unapambana na zoea la kutazama ponografia? Je, kuna lolote unaloweza kufanya ili kuacha zoea hilo? Biblia hutoa tumaini! Kabla ya kumjua Kristo, baadhi ya Wakristo wa awali walikuwa waasherati, wazinzi, na wenye pupa. Hata hivyo, Paulo alisema, “lakini mmeoshwa mkawa safi.” Hilo liliwezekanaje? Paulo ajibu: “Mmetakaswa . . . kwa roho ya Mungu wetu.”—1 Wakorintho 6:9-11.

      Usipuuze kamwe nguvu za roho takatifu ya Mungu. “Mungu ni mwaminifu,” yasema Biblia, “naye hatawaacha nyinyi mshawishwe kupita vile mwezavyo kuhimili.” Kwa kweli, ataandaa njia ya kutokea. (1 Wakorintho 10:13) Kusali kwa bidii—kumwambia Mungu shida zako daima—kutakuwa na matokeo mazuri. Neno lake hutia moyo hivi: “Umtwike BWANA mzigo wako naye atakutegemeza.”—Zaburi 55:22.

      Bila shaka, lazima utende kupatana na sala zako. Unahitaji kuazimia kutoka moyoni kukataa ponografia. Rafiki unayemtumaini au mshiriki wa familia anaweza kukusaidia sana, akikupa utegemezo na kitia-moyo unachohitaji ili kushikamana na azimio lako. (Ona sanduku “Kupata Msaada.”) Kukumbuka kwamba hatua hiyo itampendeza Mungu kwaweza kukusaidia uendelee kushikamana na azimio lako. (Mithali 27:11) Kwa kuongezea, kujua kwamba kutazama ponografia kunamchukiza Mungu kwaweza pia kukuchochea uache zoea hilo. (Mwanzo 6:5, 6) Haitakuwa rahisi, lakini unaweza kufaulu. Unaweza kuacha zoea la ponografia!

  • Madhara Yanayosababishwa na Ponografia
    Amkeni!—2003 | Julai 22
    • [Sanduku/Picha katika ukurasa wa 10]

      Kupata Msaada

      Pambano la kuacha zoea la kutazama ponografia halipaswi kuchukuliwa kijuujuu tu; linaweza kuwa pambano gumu. Dakt. Victor Cline ambaye ametibu mamia ya watu wenye zoea la kutazama ponografia asema hivi: “Ahadi hazitoshi. Haitoshi kuwa na makusudio mema. [Mtu mwenye zoea la kutazama ponografia] hawezi kufaulu peke yake.” Cline asema kwamba hatua ya kwanza ya tiba ni kumhusisha mwenzi wake ikiwa amefunga ndoa. Anadai kwamba “Tiba hufaulu haraka ikiwa wote wawili wanahusishwa. Wote wawili wameumia. Wote wanahitaji msaada.”

      Ikiwa mtu ni mseja, mara nyingi rafiki mwenye kuaminika au mshiriki wa familia anaweza kumwimarisha. Haidhuru ni nani anayehusika katika tiba hiyo, Cline hutoa sheria moja thabiti: Sema waziwazi kuhusu tatizo hilo na unapotumbukia tena katika zoea hilo. “Siri ‘huua’,” yeye asema. “Huleta aibu na dhamiri mbaya.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki