Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Paradiso Ndogo
    Amkeni!—2004 | Septemba 8
    • Sehemu Inayowavutia Wapenzi wa Ndege

      Siku inayofuata, tunasafiri kwa mtumbwi kwenye Mto Hana. Wenye kututembeza wanapiga makasia polepole, huku wakitaja majina ya aina nyingi za ndege tunaowaona. Tunasikia kelele za hondohondo, anayejulikana kwa kupiga kelele kwa mabawa yake na mlio wake mkali. Aina saba kati ya aina nyingi za hondohondo huishi katika Mbuga ya Taï. Zaidi ya aina 200 za ndege hupatikana huku. Hiyo inatia ndani aina sita za mdiria, kozi, dura, kasuku, hua, njiwa, kwale, chozi, na chechele. Pia ndege maridadi asiyepatikana kwa urahisi anayeitwa narina trogon amewahi kuonekana huku. Ndege wa kiume wa jamii hiyo huwa na mabawa yanayong’aa ya kijani, kifua chekundu, na mkia wenye manyoya meupe. Tunaona ndege wengi maridadi sana, kama vile blue plantain eater, aina moja ya hua, kasuku wa kijivu, mdiria mwenye kifua cha bluu, na kwarara fulani mwenye manyoya yanayong’aa ya kijani. Mbuga ya Taï ni sehemu inayowavutia sana wapenzi wa ndege!

  • Paradiso Ndogo
    Amkeni!—2004 | Septemba 8
    • [Picha katika ukurasa wa 16]

      Ndege aina ya “narina trogon”

      [Picha katika ukurasa wa 16]

      Tai wa mtoni wa Afrika Magharibi

      [Picha katika ukurasa wa 16]

      Ndege wanaoitwa “blue plantain eater”

      [Picha katika ukurasa wa 16]

      Kwarara

      [Picha katika ukurasa wa 16]

      Mdiria mwenye kifua cha bluu

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki