-
Je, Wamjua Shafani na Familia Yake?Mnara wa Mlinzi—2002 | Desemba 15
-
-
Kazi ya kurekebisha hekalu ilipokuwa ikiendelea, “kitabu cha torati” kilipatikana, naye Shafani ‘akaanza kukisoma mbele ya mfalme.’ Yosia alishtushwa na mambo aliyosikia na hivyo akatuma wajumbe waliotumainika kwenda kwa Hulda nabii wa kike ili kupata habari kutoka kwa Yehova kuhusu kitabu hicho. Mfalme alionyesha kwamba anamtumaini Shafani na mwana wake Ahikamu kwa kuwaweka wawe miongoni mwa wajumbe hao.—2 Wafalme 22:8-14; 2 Mambo ya Nyakati 34:14-22.
-
-
Je, Wamjua Shafani na Familia Yake?Mnara wa Mlinzi—2002 | Desemba 15
-
-
Ahikamu na Gedalia
Kama tulivyotangulia kutaja, mwana wa Shafani, Ahikamu anatajwa kwa mara ya kwanza kuhusiana na wajumbe waliotumwa kwa nabii wa kike Hulda. Kichapo fulani cha kitaalamu kinasema: “Ingawa cheo cha Ahikamu hakitajwi katika Biblia ya Kiebrania, yaonekana alikuwa na cheo cha juu.”
Miaka 15 baada ya kisa hicho, maisha ya Yeremia yalikuwa hatarini. Alipowaonya watu kwamba Yehova anakusudia kuharibu Yerusalemu, “hao makuhani, na manabii, na watu wote, wakamkamata, wakisema, Bila shaka utakufa.” Basi ni nini kilichotukia? Simulizi hilo laendelea kusema: “Mkono wa Ahikamu, mwana wa Shafani, alikuwa pamoja na Yeremia, wasimtie katika mikono ya watu auawe.” (Yeremia 26:1-24) Hilo linaonyesha nini? Kichapo The Anchor Bible Dictionary kinasema: “Kisa hiki kinaonyesha kwamba Ahikamu alikuwa na mamlaka na pia, sawa na washiriki wengine wa familia ya Shafani, alimpenda Yeremia.”
-