Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Albania
    2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Vasil Gjoka pia aliwatembelea akina ndugu kwa vipindi vifupi kulingana na uwezo wake.

  • Albania
    2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Vasil Gjoka alizuru ofisi ya tawi ya Ugiriki ambako alikaa kwa muda fulani akijifunza jinsi ya kupanga kazi ya kuhubiri. Kwa kuwa hakujua Kigiriki vizuri, ndugu waliojua Kialbania kidogo walimfundisha Vasil kwa kadiri walivyoweza. Aliporudi Tiranë, Vasil alitumia kwa bidii yote aliyokuwa amejifunza na kujaribu kupanga vizuri zaidi mikutano miwili iliyokuwa ikifanywa kila juma. Mkutano mmoja ulikuwa funzo la gazeti la Mnara wa Mlinzi la Kialbania, lililokuwa limeanza kuchapishwa karibuni.

  • Albania
    2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Katika ofisi ya tawi huko Roma, ndugu kutoka Ugiriki na Italia waliwapasha habari akina DiGregorio kuhusu hali nchini Albania na kuwaonyesha picha za baadhi ya akina ndugu wa Albania, kutia ndani Vasil Gjoka.

  • Albania
    2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Michael na Linda walipokuwa wakitembea kutoka katika uwanja wa ndege, familia ya Michael ilikuja mbio kuwalaki. Wakati huohuo, Michael akamtambua Vasil Gjoka, aliyekuwa ameelezwa kwamba akina DiGregorio wanawasili siku hiyo.

      “Wewe nenda na familia,” Michael akamwambia Linda, “naja sasa hivi.”

      Baada ya kumkumbatia Linda, watu wa familia wakabeba mizigo ya akina DiGregorio na kuharakisha kuelekea kwenye magari, huku Michael akienda haraka kukutana na Vasil.

      “Nitarudi Tiranë Jumapili,” Michael akamwambia Vasil akiwa na haraka, “tutaonana.”

  • Albania
    2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • “Tulipofika Tiranë, hatukuipata nyumba ya Vasil,” akumbuka Michael, “kwa sababu barabara hazikuwa na majina. Kwa hiyo, Koço akapendekeza tuulizie kwenye ofisi ya posta.”

      “Aliporudi kutoka posta,” asema Linda, “Koço alikuwa ameduwaa, nasi tukaenda moja kwa moja hadi nyumbani kwa Vasil.”

      Baadaye, Koço akaeleza: “Nilipoingia posta na kumuulizia Vasil, waliniambia: ‘Mtu huyo ni mtakatifu! Una habari amepatwa na nini? Tiranë nzima, hakuna mtu mwadilifu kama huyo!’ Niliposikia hivyo, nikajua kwamba Mungu alikuwa nanyi katika safari yenu! Siwezi kuwazuia!”

      KUPANGA MAMBO TIRANË

      Vasil alifurahi sana kuwaona akina DiGregorio, nao walizungumza kwa saa nyingi. Jioni ndipo Vasil alipowaeleza kwamba Jani Komino, aliyekuwa amefungwa pamoja na Nasho Dori, alikufa asubuhi hiyo. Kwa nini Vasil hakwenda kwenye mazishi ya ndugu huyo mpendwa aliyekuwa rafiki yake mkubwa? “Kwa sababu,” akaeleza, “nilikuwa nasubiri mtu aliyetumwa na Baraza Linaloongoza.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki