-
Albania2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Nilizungumza na Ilma Tani. Muda mfupi baadaye, aliruhusiwa kuja darasani. Kikundi chetu kidogo cha watu 15 kikaongezeka upesi.
Mnamo Aprili 1992, Michael na Linda DiGregorio walizuru Berat. Ilipendekezwa tualike watu wote waje kusikiliza hotuba ya Ndugu DiGregorio. Watu 54 wakahudhuria. Hakuna hata mmoja kati yetu aliyekuwa amebatizwa. Baada ya hotuba hiyo, tulikuwa na maswali mengi ya kuwauliza Ndugu na Dada DiGregorio. Hatimaye tukajua jinsi tunavyopaswa kutimiza huduma yetu.
Muda mfupi baadaye, Mashahidi wa Yehova wakatambuliwa rasmi kisheria. Ilma nami pamoja na ndugu wawili tukaenda Tiranë kujifunza jinsi ya kuhubiri nyumba kwa nyumba. Tuliombwa tutakaporudi Berat tuwafundishe wengine. Tulijitahidi sana. Mapainia wa pekee wanne kutoka Italia walipopewa mgawo wa kwenda Berat, mnamo Machi 1993, kutaniko lilipiga hatua, na kuanza kufanya mikutano miwili kila juma.
Mwezi huo wa Machi, Ilma pamoja nami tulibatizwa katika kusanyiko la pekee lililofanywa Tiranë. Watu 585 walihudhuria. Tukaanza upainia wa kawaida na baada ya muda tukawekwa kuwa mapainia wa pekee wa kwanza wenyeji. Sasa tulikuwa na uhuru wa kufanya mambo. Tukapewa mgawo wa kwenda Korçë.
Baadaye, Ilma akaolewa na Arben Lubonja, aliyekuwa akihubiri Korçë akiwa peke yake. Mwishowe, wakaanza kufanya kazi ya mzunguko, na sasa wanatumikia Betheli. Nafurahi kwamba nilimwalika Ilma!
-
-
Albania2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha]
Ilma (Tani) na Arben Lubonja
-