-
Albania2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Mwaka wa 1992, mapainia wa pekee waliwasili kutoka Italia na Ugiriki, na kuhudhuria mtaala wa kujifunza Kialbania. Wakati huohuo, kikundi kidogo kikaanza kutafsiri vitabu vyetu.
-
-
Albania2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Huku kuni zikiendelea kutemwa na mitaala ya lugha ikiendelea, kikundi cha watafsiri wa Kialbania walitembelewa kwa mara ya kwanza na Nick na Amy Ahladis kutoka katika Huduma za Tafsiri, Patterson, New York. Ndugu na Dada Ahladis waliwatembelea tena baadaye mara kadhaa. Mtazamo wao wenye fadhili na usawaziko uliwasaidia watafsiri hao wapya, nao wakajifunza haraka na kufanya kazi nzuri. Ofisi ya tawi ya Italia ilikuwa ikichapa vitabu na kuvituma Albania.
-