Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Albania
    2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • [Sanduku/Picha katika ukurasa wa 173, 174]

      Mwisho wa Kufanya Mikutano Kisiri

      ADRIANA MAHMUTAJ

      ALIZALIWA 1971

      ALIBATIZWA 1993

      MAELEZO MAFUPI KUMHUSU Alialikwa kuhudhuria mkutano uliofanywa kisiri, halafu mambo yakabadilika ghafula. Sasa anatumikia akiwa painia wa pekee.

      ◼ BINAMU yangu alipokufa mwaka wa 1991, nilimsikia mwanamke aitwaye Barie, akitumia Biblia kumtia moyo shangazi yangu. Mara moja nikaanza kuuliza maswali, kisha nikaombwa nikutane na rafiki yake, Rajmonda kazini kwao. Familia ya kina Rajmonda ilikuwa ikifanya mikutano katika “darasa.” Rajmonda alinieleza kwamba sina budi kujifunza Biblia kwa muda, kwa sababu wapya hawaruhusiwi kuingia katika darasa hilo mara moja. Nilipendezwa sana na mambo niliyokuwa nikijifunza, na muda si muda, nikaruhusiwa kuhudhuria.

      Darasa hilo lilikuwa na watu ambao hawakuwa wamebatizwa, waliokuwa wakikutanika pamoja na Sotir Papa na Sulo Hasani hapo awali. Miaka kadhaa mapema, maofisa wa Sigurimi walikuwa wamepenya kisiri na kuwasaliti akina ndugu kwa polisi. Kwa hiyo, wote walijiendesha kwa tahadhari nao walikuwa waangalifu sana kabla ya kumwalika mtu yeyote ahudhurie mikutano!

      Katika mkutano wa kwanza niliohudhuria, nilipata kujua kwamba tunapaswa kuwa na orodha ya rafiki zetu na kuwaambia mambo tunayojifunza. Nilizungumza na Ilma Tani. Muda mfupi baadaye, aliruhusiwa kuja darasani. Kikundi chetu kidogo cha watu 15 kikaongezeka upesi.

      Mnamo Aprili 1992, Michael na Linda DiGregorio walizuru Berat. Ilipendekezwa tualike watu wote waje kusikiliza hotuba ya Ndugu DiGregorio. Watu 54 wakahudhuria. Hakuna hata mmoja kati yetu aliyekuwa amebatizwa. Baada ya hotuba hiyo, tulikuwa na maswali mengi ya kuwauliza Ndugu na Dada DiGregorio. Hatimaye tukajua jinsi tunavyopaswa kutimiza huduma yetu.

      Muda mfupi baadaye, Mashahidi wa Yehova wakatambuliwa rasmi kisheria. Ilma nami pamoja na ndugu wawili tukaenda Tiranë kujifunza jinsi ya kuhubiri nyumba kwa nyumba. Tuliombwa tutakaporudi Berat tuwafundishe wengine. Tulijitahidi sana. Mapainia wa pekee wanne kutoka Italia walipopewa mgawo wa kwenda Berat, mnamo Machi 1993, kutaniko lilipiga hatua, na kuanza kufanya mikutano miwili kila juma.

  • Albania
    2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Ingawa mamia ya kina ndugu wamehama kutoka Berat kwa sababu za kiuchumi, kikundi kidogo kilichokuwapo sasa kimepanuka na kuwa makutaniko matano makubwa!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki