-
Albania2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Aprili 1997, wanajeshi 7,000 wa vikosi vya Umoja wa Mataifa walifika ili kurejesha utulivu nchini. Kufikia Agosti, wanajeshi hao walikuwa wameondoka Albania, na ikawezekana kwa akina ndugu kupanga kusanyiko la wilaya. Wahubiri walifurahi sana; kwa kuwa kwa miezi mingi walikuwa wakikutanika katika vikundi vidogo-vidogo tu.
Wanyang’anyi wenye silaha walizuilia baadhi ya mabasi yaliyokodiwa na akina ndugu ili kuwapeleka kusanyikoni. Hata hivyo, walipojua kwamba abiria hao ni Mashahidi wa Yehova, walisema: “Ninyi watu mko tofauti! Hatuwezi kuwadhuru.”
-
-
Albania2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Kwenye kusanyiko la 2000, wahudhuriaji Waalbania walipata zawadi ya pekee. Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo ilitangazwa katika Kialbania! Kikundi cha watafsiri wenye bidii kilijikakamua kuukamilisha mradi huo katika muda unaopungua mwaka mmoja. Painia wa kawaida aliyekuwa mbunge Mkomunisti awali aliandika: “Ni jambo lenye kupendeza kama nini! Baada ya kuichunguza tafsiri hii, ndipo tu nimetambua jinsi Biblia hii inavyopendeza, lugha yake sanifu, ushairi, na masimulizi yenye kupendeza. Niliposoma jinsi Yesu alivyofanya miujiza na jinsi alivyokemewa na kudhihakiwa, hisia nyingi sana ziliibuka moyoni, hisia ambazo sijawahi kuwa nazo. Niliviona waziwazi akilini vikao vyote vyenye kuchochea hisia!”
-