Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Neno la Yehova Laenea Katika “Nchi ya Tai”
    Mnara wa Mlinzi—2005 | Oktoba 15
    • Mapainia Wenye Bidii Kutoka Nchi Nyingine Waongoza Kazi

      Mapema mnamo 1992, Baraza Linaloongoza lilifanya mipango ili Michael na Linda DiGregorio, wenzi wa ndoa wamishonari wenye asili ya Kialbania, wasafiri kwenda Albania. Waliwasiliana na Mashahidi waaminifu wenye umri mkubwa, nao wakawasaidia kuungana tena katika undugu wa ulimwenguni pote. Kikundi chenye bidii cha mapainia wa pekee 16, au waeneza-injili wa wakati wote, kutoka Italia, kilifika mnamo Novemba, pamoja na mapainia wanne kutoka Ugiriki. Mipango ilifanywa ili kuwasaidia wajifunze Kialbania.

      Mapainia hao wageni walikabili hali ngumu. Umeme haukupatikana kwa ukawaida. Katika majira ya baridi kali kulikuwa na baridi na unyevu. Watu walipiga foleni kwa saa nyingi ili kupata chakula na mahitaji mengine ya maisha. Hata hivyo, tatizo kubwa zaidi ambalo ndugu hao walikabili lilikuwa jinsi ya kupata nyumba kubwa vya kutosha ili kukaribisha umati mkubwa wa watu waliopendezwa na kweli!

      Mapainia waliokuwa wakijitahidi kujifunza Kialbania waligundua kwamba kujua lugha ni njia ya kuwasilisha tu ujumbe. Mwalimu mmoja wa Biblia mwenye uzoefu aliwaambia hivi: “Hatuhitaji kuzungumza kupatana na sarufi ili kutabasamu kwa shauku au kuwakumbatia ndugu zetu. Waalbania wataitikia upendo ambao mnaonyesha kutoka moyoni mwenu wala si kuzungumza kwa usahihi kupatana na sarufi. Msijali, wataelewa.”

      Baada ya kipindi cha kwanza cha kujifunza lugha, mapainia walianza kuhubiri huko Berat, Durres, Gjirokastër, Shkodër, Tiranë, na Vlorë. Punde si punde, makutaniko yalianzishwa katika majiji hayo. Areti Pina, aliyekuwa na umri wa zaidi ya miaka 80 na ambaye alikuwa na matatizo ya afya, alikuwa bado huko Vlorë. Mapainia wa pekee wawili walitumwa kuhubiri na Areti. Watu walishangaa kuona wageni wakizungumza Kialbania: “Wamishonari wa dini nyingine wanatuambia kwamba ili tujifunze jambo lolote tunapaswa kujifunza kwanza Kiingereza au Kiitaliano. Kwa kuwa ninyi mmejifunza Kialbania, ni wazi kwamba mnatupenda sana na kwamba mna ujumbe muhimu!”

  • Neno la Yehova Laenea Katika “Nchi ya Tai”
    Mnara wa Mlinzi—2005 | Oktoba 15
    • [Picha katika ukurasa wa 19]

      Kikundi cha kwanza cha mapainia wageni wakihudhuria masomo ya kujifunza lugha

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki