-
Albania2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Katika miaka ya 1950, mambo yalikuwa magumu hata zaidi. Chuki ya kisiasa kati ya Albania na Ugiriki iliongezeka. Uhusiano wa kidplomasia kati ya Albania na nchi za Uingereza na Marekani ulikuwa umevunjika. Isitoshe, uhusiano wa Albania na Muungano wa Sovieti ulikuwa mashakani. Albania ilianza kujitenga na kujitegemea. Mawasiliano yote yalikuwa yakipigwa darubini.
-
-
Albania2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Mwaka wa 1959 Wizara ya Haki ilivunjwa, nao wanasheria hawakuruhusiwa kuendelea kufanya kazi. Chama cha Kikomunisti kiliunda na kutekeleza sheria zote. Wale ambao hawakupiga kura walionwa kuwa adui. Hali ya woga na wasiwasi ilikuwa imetanda.
-