-
Albania2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Kosta Dabe alikuwa nchini Ugiriki tangu 1966 akijaribu kutafuta kibali cha kurudi nyumbani kwao, Albania. Akiwa na umri wa miaka 76, alitaka kuwafundisha watoto wake kweli. Alipokosa kibali, Kosta aliacha pasipoti yake ya Marekani kwenye mpaka wa Albania na kuingia nchini, akijua kwamba huenda asiweze kamwe kutoka.
-
-
Albania2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Novemba 1976 barua kutoka kwa Kosta Dabe iliripoti kwamba watu watano walihudhuria Ukumbusho huko Vlorë. Alijua kwamba kulikuwa na Mashahidi wawili, ambao kila mmoja wao alifanya Ukumbusho akiwa peke yake, mmoja mjini Përmet na mwingine Fier. Mjini Tiranë, Ukumbusho ulifanyiwa sehemu mbili, wawili walikutanika sehemu moja na wanne wakakutanika sehemu nyingine. Hivyo, kwa kutegemea habari alizojua, hudhurio la Ukumbusho mwaka wa 1976 lilikuwa angalau watu 13.
-