Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Albania
    2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • ALIKUWA NA IMANI YENYE NGUVU HADI MWISHO

      Nasho Dori, akiwa na umri wa miaka 80 na kitu, alikuwa mgonjwa na dhaifu. Lakini kikundi kimoja cha akina ndugu kilihitaji sana kutiwa moyo naye—vijana waliotakiwa kujiunga na jeshi. Makasisi wa Kiothodoksi huko Berat, ambao waliona kijicho kwa sababu ya ongezeko la Mashahidi wa Yehova, waliwashinikiza wenye mamlaka wawafunge vijana hao.

      Ndugu sita vijana waliokataa kujiunga na jeshi wangeweza kufungwa miezi kadhaa. Akijua kwamba wanahitaji kutiwa moyo, Nasho aliketi kitandani na kurekodi ujumbe kwenye video kwa ajili yao.

      “Msiogope,” Nasho akawahimiza ndugu hao vijana. “Haitakuwa mara ya kwanza. Yehova atakuwa nanyi. Mkitupwa gerezani, msiwe na wasiwasi. Hatimaye jina la Yehova litatukuzwa.”

      Afya ya Nasho ilipozidi kuzorota, aliwaita akina ndugu na kuwaambia: “Nimemwomba Yehova msamaha. Juma lililopita nilikuwa na maumivu makali sana hivi kwamba nikaomba nife. Kisha nikawaza, ‘Yehova, wewe ndiwe Chanzo cha uhai. Uhai una thamani sana machoni pako. Nilikuwa nikiomba kitu ambacho ni kinyume cha mapenzi yako. Tafadhali nisamehe!’”

      Nasho alipopata habari kwamba idadi ya wahubiri nchini Albania imefikia 942, akasema: “Hatimaye tumepata umati mkubwa nchini Albania!” Siku chache baadaye, akafa, akiwa na tumaini la kutawala pamoja na Yesu mbinguni.

  • Albania
    2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • [Picha katika ukurasa wa 186]

      “Mkitupwa gerezani, msiwe na wasiwasi.”—Nasho Dori

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki