Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mtazamo Unaofaa Kuhusu Pombe
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Januari 1
    • Allen anasema: “Nilipokuwa nikijitahidi kuacha pombe, nilipatwa na maumivu makali sana. Ndipo nilipotambua kwamba ingawa nilikuwa nikipata msaada wa kiroho, nilihitaji pia matibabu.”

  • Mtazamo Unaofaa Kuhusu Pombe
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Januari 1
    • Miaka 24 baada ya kuacha pombe, Allen anasema hivi: “Nilifurahi sana nilipojua kwamba ninaweza kubadilika, na kujua kwamba Yehova alitaka kunisaidia kurekebisha mambo yaliyokuwa yameenda kombo maishani mwangu, na kwamba yeye . . . ” Allen anatua ili kuzuia machozi yanayotaka kububujika anapokumbuka mambo ya zamani. “Yaani, . . . ni jambo zuri sana kujua kwamba Yehova anaelewa, anajali, na anasaidia.”

  • Mtazamo Unaofaa Kuhusu Pombe
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Januari 1
    • [Sanduku/Picha katika ukurasa wa 10]

      Neno la Mungu Lamsaidia Mtu Aliyekuwa Mlevi

      Supot anayeishi nchini Thailand alikuwa mlevi. Mwanzoni alikuwa akinywa jioni tu. Hatimaye alianza kunywa asubuhi na pia wakati wa pumziko la mchana. Mara nyingi alikunywa kusudi tu alewe. Kisha, akaanza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Supot aliacha kunywa alipojifunza kwamba Yehova Mungu hakubali ulevi. Lakini, baada ya muda akarudia ulevi. Watu wa familia yake walihuzunika sana.

      Hata hivyo, Supot bado alimpenda Yehova na alitaka kumwabudu ifaavyo. Marafiki wa Supot waliendelea kumsaidia na kuwatia moyo watu wa familia yake watumie wakati mwingi zaidi pamoja naye, na wasiache kumsaidia. Wakati huo, andiko la 1 Wakorintho 6:10 linalosema wazi kwamba ‘walevi hawataurithi ufalme wa Mungu,’ lilimsaidia Supot kuona umuhimu wa kuacha ulevi. Alitambua kwamba alihitaji kufanya jitihada ya kufa na kupona ili kuacha ulevi.

      Supot aliazimia kuacha kabisa kunywa pombe. Hatimaye, kwa nguvu za roho takatifu ya Mungu, mwongozo wa Neno la Mungu, na msaada wa watu wa familia na ndugu kutanikoni, Supot alipata nguvu za kiroho na akashinda tamaa ya pombe. Watu wa familia yake walifurahi sana alipobatizwa ili kuonyesha kwamba alikuwa amejiweka wakfu kwa Mungu. Sasa Supot ana ule uhusiano wa karibu pamoja na Mungu ambao alitamani kuwa nao tangu zamani, na anatumia wakati wake kuwasaidia wengine kiroho.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki