Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ‘Nafsi Zilizochinjwa’ Zathawabishwa
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • “Na wakati alipofungua kifungo cha tano, mimi nikaona chini-chini ya madhabahu nafsi za wale waliochinjwa kwa sababu ya Neno la Mungu na kwa sababu ya kazi ya ushuhuda ambayo walizoea kuwa nayo.” (Ufunuo 6:9, NW)

  • ‘Nafsi Zilizochinjwa’ Zathawabishwa
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 3. (a) Kwenye tabenakulo ya Kiyahudi ya kale, nafsi zilimwagwaje “penye msingi wa madhabahu”? (b) Ni kwa nini Yohana aliona nafsi za mashahidi waliochinjwa zikiwa chini-chini ya madhabahu ya ufananisho katika mbingu?

      3 Chini-chini ya madhabahu hii ziko “nafsi za wale waliochinjwa kwa sababu ya Neno la Mungu na kwa sababu ya kazi ya ushuhuda ambayo walizoea kuwa nayo.” Hii humaanisha nini? Hizi hazingekuwa nafsi zilizoachanishwa na mwili—kama zile walizoamini Wagiriki wapagani. (Mwanzo 2:7; Ezekieli 18:4, ZSB) Badala ya hivyo, Yohana anajua kwamba nafsi, au uhai, hufananishwa na damu, na wakati makuhani kwenye tabenakulo ya kale ya Kiyahudi walipochinja mnyama wa dhabihu, wao walinyunyiza damu “kuzunguka pande zote juu ya madhabahu” au “penye msingi wa madhabahu ya toleo la kuteketezwa.” (Walawi 3:2, 8, 13; 4:7; 17:6, 11, 12, NW) Kwa sababu hiyo, nafsi ya mnyama ilishirikishwa karibu-karibu na madhabahu. Lakini ni kwa sababu gani nafsi, au damu, za hawa watumishi wa Mungu hasa zionwe chini-chini ya madhabahu ya ufananisho katika mbingu? Ni kwa sababu kifo chao huonwa kuwa cha kidhabihu.

      4. Ni katika njia gani kifo cha Wakristo waliozaliwa kwa roho ni cha kidhabihu?

      4 Kweli kweli, wale wote wanaozaliwa kuwa wana wa roho wa Mungu wanakufa kifo cha kidhabihu. Kwa sababu ya daraka wanalopaswa kushiriki katika Ufalme wa Yehova wa kimbingu, ni mapenzi ya Mungu kwamba wakane kabisa kabisa na wadhabihu tumaini lolote la uhai wa milele duniani. Katika njia hii, wao wanajitiisha kwenye kifo cha kidhabihu kwa ajili ya enzi kuu ya Yehova. (Wafilipi 3:8-11; linga 2:17.) Hiyo ni kweli katika maana halisi kabisa kwa habari ya wale ambao Yohana aliona chini ya madhabahu. Wao walikuwa wapakwa-mafuta ambao katika siku yao walifia imani kwa ajili ya huduma yao ya bidii katika kutegemeza Neno na enzi kuu ya Yehova. ‘Nafsi zao zilichinjwa kwa sababu ya Neno la Mungu na kwa sababu ya kazi ya ushuhuda [mar·ty·riʹan] ambayo walizoea kuwa nayo.’

      5. Ni kwa jinsi gani nafsi za waaminifu, zijapokuwa zimekufa, zinalia kwa sauti kubwa ili kisasi kilipwe?

      5 Ule mfululizo wa mandhari waendelea kufunguka: “Na hizo zikalia kwa sauti kubwa, zikisema: ‘Ni mpaka lini, Bwana Mwenye Enzi Kuu mtakatifu na wa kweli, wewe unajizuia usihukumu na kulipiza kisasi damu yetu juu ya wale ambao wanakaa juu ya dunia?’” (Ufunuo 6:10, NW) Nafsi zao, au damu, zingeweza kuliaje kwa kutaka kisasi, kwa kuwa Biblia inaonyesha kwamba wafu hawana fahamu? (Mhubiri 9:5) Basi, je! damu ya Abeli mwadilifu haikulia kwa sauti kubwa wakati Kaini alipomwua kimakusudi? Ndipo Yehova alipomwambia Kaini hivi: “Wewe umefanya nini? Sikiliza! Damu ya ndugu yako inanililia mimi kwa sauti kubwa kutoka ardhi.” (Mwanzo 4:10, 11, NW; Waebrania 12:24) Si kwamba damu ya Abeli ilikuwa ikitamka maneno kihalisi. Badala ya hivyo, Abeli alikuwa amekufa akiwa jeruhi asiye na hatia, nayo haki ililia kwa sauti kubwa ikitaka mwuaji kimakusudi wake aadhibiwe. Hali moja na hiyo, Wakristo hao wafia-imani hawana hatia, na kwa haki lazima walipiwe kisasi. (Luka 18:7, 8) Kilio cha kutaka kisasi kilipwe ni kikuu kwa sababu maelfu wengi wamekufa.—Linga Yeremia 15:15, 16.

      6. Ni umwagaji-damu gani usio na hatia uliolipizwa kisasi katika 607 K.W.K.?

      6 Hali hiyo ingeweza kufananishwa pia na ile iliyokuwa Yuda yenye kuasi imani wakati Mfalme Manase alipokuja kukalia kiti cha ufalme katika 716 K.W.K. Yeye alimwaga damu nyingi isiyo na hatia, pengine ‘akimpasua vipande vipande kwa msumeno’ nabii Isaya. (Waebrania 11:37, NW; 2 Wafalme 21:16) Ijapokuwa baadaye Manase alitubu na akabadilika, hiyo hatia ya damu ilibaki. Katika 607 K.W.K., wakati Wababuloni walipouacha ukiwa ufalme wa Yuda, “ilikuwa tu kwa amri ya Yehova kwamba hilo likatukia dhidi ya Yuda, kuiondoa machoni pake kwa ajili ya madhambi ya Manase, kulingana na yale yote ambayo yeye alikuwa amefanya; na pia kwa ajili ya damu isiyo na hatia ambayo yeye alikuwa amemwaga, hivi kwamba yeye alijaza Yerusalemu damu isiyo na hatia, na Yehova hakuidhini kutoa msamaha.”—2 Wafalme 24:3, 4, NW.

      7. Ni nani hasa mwenye hatia ya ‘umwagaji-damu ya watakatifu’?

      7 Kama vile katika nyakati za Biblia, ndivyo na leo, wengi wa wale watu mmoja mmoja walioua mashahidi wa Mungu huenda wamekufa kitambo. Lakini tengenezo lililosababisha ufia-imani wao lingali hai sana na ni lenye hatia ya damu. Ni tengenezo la Shetani la kidunia, mbegu yake ya kidunia. Sehemu yenye kutokeza katika hiyo ni Babuloni Mkubwa, ile milki ya ulimwengu ya dini bandia.a Yeye anaelezwa kuwa ‘amelewa kwa damu ya watakatifu na kwa damu ya mashahidi wa Yesu.’ Ndiyo, “katika yeye ilipatikana damu ya manabii na ya watakatifu na ya wale wote ambao wamechinjwa juu ya dunia.” (Ufunuo 17:5, 6; 18:24; Waefeso 4:11; 1 Wakorintho 12:28, NW) Ni mzigo wa hatia ya damu kama nini! Maadamu Babuloni Mkubwa yupo, damu ya majeruhi wake italia kwa sauti kubwa kwa kutaka haki itekelezwe.—Ufunuo 19:1, 2.

      8. (a) Ni mifano gani ya ufia-imani iliyokuwa imetukia wakati wa maisha ya Yohana? (b) Ni minyanyaso gani iliyochochewa na wamaliki Waroma?

      8 Yohana mwenyewe alishuhudia ufia-imani katika karne ya kwanza wakati Nyoka mkatili na mbegu yake ya kidunia walipopiga vita juu ya kundi la Wakristo wapakwa-mafuta lililokuwa likikua. Yohana alikuwa ameona Bwana yetu akitundikwa juu ya nguzo na alikuwa ameishi kupitia vipindi vya kuuawa kwa Stefano, kwa ndugu yake mwenyewe Yakobo, na kwa Petro, kwa Paulo, na washiriki wengine wa karibu. (Yohana 19:26, 27; 21:15, 18, 19; Matendo 7:59, 60; 8:2; 12:2; 2 Timotheo 1:1; 4:6, 7) Katika 64 W.K., Nero, maliki Mroma alikuwa amelaumu bure Wakristo, akiwashtakia kuteketeza jiji, ili kukanusha uvumi wa kwamba ndiye aliyekuwa mwenye hatia. Mwanahistoria Takito anaripoti hivi: “Wao [Wakristo] walikufa kwa njia za dhihaka; baadhi yao walifunikwa ngozi za hayawani-mwitu kisha wakararuliwa na mbwa, baadhi yao [walitundikwa juu ya nguzo],b baadhi yao walichomwa kuwa mienge ya kunurisha usiku.” Wimbi zaidi la mnyanyaso chini ya Maliki Domitiano (81-96 W.K.) lilikuwa limetokeza kuhamishwa kwa Yohana kupelekwa kisiwa cha Patmosi. Kama Yesu alivyosema: “Ikiwa wao wamenyanyasa mimi, wao watanyanyasa nyinyi pia.”—Yohana 15:20; Mathayo 10:22, NW.

      9. (a) Ni kipeo gani cha udanganyifu alichotokeza Shetani kufikia karne ya nne W.K., nacho ni sehemu kuu ya nini? (b) Baadhi ya watawala wa Jumuiya ya Wakristo waliwatendeaje Mashahidi wa Yehova wakati wa Vita ya Ulimwengu 1 na 2?

      9 Kufikia karne ya nne W.K., yule nyoka wa zamani, Shetani Ibilisi, alikuwa ametokeza kipeo cha udanganyifu wake, ile dini yenye uasi-imani ya Jumuiya ya Wakristo—mfumo wa Kibabuloni uliofichwa chini ya kibandiko cha “Ukristo.” Ndiyo sehemu iliyo kuu ya mbegu ya yule Nyoka na imesitawi ikawa umati wa farakano zenye kuhitilafiana. Kama Yuda ya kale isiyo na imani, Jumuiya ya Wakristo inabeba hatia nzito ya damu, ikiwa imekwisha kujihusisha sana katika pande zote mbili za Vita ya Ulimwengu 1 na 2. Wengine wa watawala wa kisiasa wa Jumuiya ya Wakristo hata walitumia vita hivyo kuwa kisababu cha kuchinja watumishi wa Mungu. Likiripoti juu ya Hitla kunyanyasa Mashahidi wa Yehova, pitio la kitabu Kirchenkampf in Deutschland (Vita ya Makanisa Katika Ujeremani) lilitaarifu hivi: “Theluthi moja yao [Mashahidi] waliuawa, ama walifishwa kwa amri ya kiserikali, ama kwa matendo mengine ya jeuri, njaa, ugonjwa au kazi ngumu ya utumwa. Ukali wa utiisho huu ulikuwa bila kitangulizi na ulikuwa tokeo la imani thabiti ambayo haingeweza kupatanishwa na siasa ya Usoshalisti wa Kitaifa.” Kweli kweli, inaweza kusemwa juu ya Jumuiya ya Wakristo, kutia na upadri wayo: “Katika marinda yako zimepatikana alama za damu ya nafsi za maskini wasio na hatia.”—Yeremia 2:34, NW.c

  • ‘Nafsi Zilizochinjwa’ Zathawabishwa
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • “Na joho jeupe lilipewa kwa kila mmoja wao; na wao waliambiwa wapumzike kwa kitambo kidogo zaidi, mpaka hesabu ilipokuwa imejazwa pia ya watumwa wenzao na ndugu zao ambao walikuwa karibu kuuawa kama wao pia walivyokuwa.” (Ufunuo 6:11, NW) Kupokea kwao “joho jeupe” kunahusiana na kufufuliwa kwao wakawe viumbe wa roho wasioweza kufa. Hawalali tena wakiwa nafsi zilizochinjwa chini-chini ya madhabahu, bali wanainuliwa wakawe sehemu ya kile kikundi cha wazee 24 ambao huabudu mbele ya kiti cha ufalme cha Mungu. Huko, wao wenyewe wamepewa viti vya ufalme, kuonyesha kwamba wao wamekwisha ingia katika mapendeleo ya kifalme. Na “wamevalia mavazi ya nje meupe,” kuashiria kwamba wao wamekwisha hukumiwa kuwa waadilifu, wastahilio mahali pa heshima mbele za Yehova katika kitala cha kifalme. Hilo pia ni katika utimizo wa ahadi ya Yesu kwa Wakristo wapakwa-mafuta waaminifu katika kundi la Sardisi: “Yeye ambaye hushinda atapambwa hivyo kwa mavazi ya nje meupe.”—Ufunuo 3:5; 4:4; 1 Petro 1:4, NW.

      12. Ni katika njia gani Wakristo waliofufuliwa ‘hupumzika kwa kitambo kidogo zaidi,’ na mpaka lini?

      12 Ithibati yote huonyesha kwamba ufufuo huu wa kimbingu ulianza katika 1918, baada ya Yesu kuketishwa juu ya kiti cha ufalme katika 1914 na kutoka kwake aende akipanda farasi kuanza ushindi wake wa kifalme kwa kuzisafisha mbingu watoke Shetani na roho waovu wake. Hata hivyo, wapakwa-mafuta hao waliofufuliwa wanaambiwa kwamba lazima “wapumzike kwa kitambo kidogo zaidi, mpaka hesabu . . . pia ya watumwa wenzao” ijazwe. Wale wa jamii ya Yohana ambao wangali duniani lazima wathibitishe ukamilifu wao chini ya jaribu na mnyanyaso, na huenda baadhi ya hawa bado wakauawa. Hata hivyo, mwishowe, damu yote yenye uadilifu iliyomwagwa na Babuloni Mkubwa na hawara zake wa kisiasa italipiwa kisasi. Kwa wakati uliopo, pasipo shaka wale waliofufuliwa wana shughuli wakiwa na wajibu mwingi wa kimbingu. Wao wanapumzika, si kwa kustarehe katika raha ya kutotenda, bali katika njia ya kwamba wao wanangojea kwa subira siku ya kisasi cha Yehova. (Isaya 34:8; Warumi 12:19) Pumziko lao litakwisha wakati wao watashuhudia uharibifu wa dini bandia na, wakiwa ‘walioitwa na waliochaguliwa na waaminifu,’ wao wanaandamana na Bwana Yesu Kristo katika kutekeleza hukumu hapa duniani juu ya sehemu nyingine zote za mbegu mbovu ya Shetani.—Ufunuo 2:26, 27; 17:14; Warumi 16:20.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki