Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Samoa
    2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • WAMISHONARI WA GILEADI WAWASILI

      Mnamo Februari 4, 1955, wamishonari Paul na Frances Evans, na pia Gordon na Patricia Scott kutoka Marekani, walifika Samoa ya Marekani. Waliishi katika makao ya wamishonari ya Fagatogo. Kutoka katika makao hayo, mtu angeweza kuona watu na pilikapilika zao za kila siku kijijini. Leonard (Len) Helberg, mwangalizi wa mzunguko aliyetembelea Pago Pago mwaka huo asimulia mambo aliyojionea:

      “Wamishonari walikuwa wakikaa katika nyumba kubwa iliyokuwa juu ya duka kubwa la zamani. Upande mmoja, ng’ambo ya kijito, kulikuwa na baa, nao mabaharia walipenda kujiburudisha humo wakati wa jioni. Walipolewa na kuanza kusababisha vurugu barabarani, polisi wa kijiji hicho, ambaye alikuwa mfupi lakini ngangari, angejipenyeza katikati ya umati huo akiwa na sigara yake mdomoni huku akivurumisha makonde huku na huku ili kutenganisha pande mbili zinazozozana. Upande wa nyuma wa nyumba hiyo, kutoka katika kanisa lililokuwa likipakana na nyumba yetu kulikuwa na kelele za mahubiri ya kuwatisha watu kuhusu moto wa mateso. Tukiwa kwenye varanda upande wa mbele, tulikuwa tukiona umati wa watu ukikusanyika karibu na benki mara moja kwa mwezi siku ya mshahara. Wamishonari kutoka katika makanisa, walikuja kutoka pande zote za kisiwa hicho ili kukusanya fungu la kumi kutoka kwa waumini wao kabla hawajatumia mishahara yao.”

      Katika mazingira hayo yenye vituko, watu wengi walipendezwa na mambo ya kiroho. Len anaeleza: “Mmishonari mmoja alikuwa akianza mahubiri saa 12 asubuhi kwa kuongoza funzo la Biblia katika kibanda cha kunyolea kilichokuwa karibu na nyumba yao, kabla kinyozi huyo kufungua kazi. Baada ya hapo, angejifunza na mwokaji mikate, kabla ya kununua mkate ambao angerudi nao nyumbani kwa ajili ya kiamsha-kinywa. Baadaye siku hiyo, ndugu huyohuyo alijifunza na kikundi cha wafungwa katika jela iliyokuwa katika kijiji hicho.” Kufikia mwisho wa mwaka huo, wamishonari hao walikuwa wakiongoza mafunzo ya Biblia 60 hivi yaliyokuwa yakihudhuriwa na watu zaidi ya 200.

  • Samoa
    2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Watu waliopendezwa hawakungoja watembelewe nyumbani na Mashahidi, badala yake walijileta wenyewe katika makao ya wamishonari, ambapo wamishonari waliongoza mafunzo kadhaa sehemu tofauti-tofauti katika makao hayo wakati uleule. Kikundi kimoja kilipoondoka kingine kiliingia. “Miaka kadhaa baadaye,” Ron Sellars anasema, “bado watu walikuwa wakihusianisha mambo waliyoona katika filamu ile na Mashahidi wa Yehova.”

  • Samoa
    2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Siku iliyofuata, nilikuwa katika maktaba ya shule wakati ambapo Ndugu Paul Evans aliingia bila mimi kumtarajia. Alipoona kwamba kuna jambo linalonisumbua, aliniambia, “Twende kwenye makao ya wamishonari, tukazungumze.” Wamishonari walinikaribisha kwa fadhili, na mwaka huohuo nikabatizwa.

      Baada ya kumaliza masomo yangu ya sekondari, nilianza kufanya upainia pamoja na wamishonari.

  • Samoa
    2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Ninathamini sana kielelezo cha wamishonari hao wa kwanza-kwanza. Walinichochea kumpenda Yehova, jambo ambalo limenitegemeza hadi leo hii!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki