-
Samoa2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
UTAMADUNI WA KISAMOA
Caroline Pedro, painia kutoka Kanada ambaye aliolewa na Wallace Pedro mwaka wa 1960, anasema: “Tulifurahia sana kuhubiri zamani hizo. Karibu katika kila nyumba kulikuwa na mtu aliyependezwa na ujumbe wa Biblia. Ilikuwa rahisi kuanzisha mafunzo ya Biblia, na mara nyingi familia nzima-nzima ziliketi kusikiliza.
“Hatuwezi kusahau jinsi ilivyokuwa tulipokuwa tukihubiri vijijini. Kwa kawaida watoto wadogo walikuwa wakitufuata kutoka nyumba moja hadi nyingine wakisikiliza kwa makini mahubiri yetu. Kisha wangekimbia hadi nyumba iliyofuata na kuwaambia kwamba tunakuja. Hata waliwaeleza wenye nyumba ujumbe wetu na maandiko tuliyokuwa tukitumia! Ili kuwaweza watoto hao, tulitayarisha aina mbalimbali za utangulizi.”
-
-
Samoa2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Caroline Pedro anasema: “Salamu hizo zilitusaidia kufahamiana na watu mbalimbali na familia zao. Hivyo tungeweza kuwasaidia vizuri zaidi kiroho.”
-
-
Samoa2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Ilikuwa kawaida kuwa na mazungumzo marefu ya Biblia kwa sababu watu wengi walikuwa wameisoma Biblia. Caroline Pedro anasema: “Mazungumzo hayo yalinisaidia kuelewa vizuri zaidi habari mbalimbali za Biblia.”
-