Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kufunika Kichwa—Wakati Gani na kwa Nini?
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
    • Kusudi. Mstari wa 10 unataja sababu mbili zinazomlazimu mwanamke Mkristo kutimiza takwa hilo: “Mwanamke anapaswa kuwa na ishara ya mamlaka juu ya kichwa chake kwa sababu ya malaika.”

  • Kufunika Kichwa—Wakati Gani na kwa Nini?
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
    • Sababu ya pili inaonyeshwa na maneno haya, “kwa sababu ya malaika.” Mwanamke anapofunika kichwa, hilo linawahusuje viumbe hao wa roho wenye nguvu?

      Malaika hupendezwa wanapoona kwamba mamlaka ya Mungu inatambuliwa katika tengenezo lote la Yehova, mbinguni na duniani. Pia, wanafaidika kutokana na mifano ambayo wanadamu wasio wakamilifu wanaweka katika jambo hilo. Ndiyo, hata malaika wanajitiisha kwa mpango wa Yehova—jambo ambalo malaika kadhaa walishindwa kufanya wakati uliopita. (Yuda 6) Huenda malaika wakamwona mwanamke Mkristo ambaye ana uzoefu mwingi, ujuzi mwingi, na akili nyingi kuliko mwanamume fulani ambaye amebatizwa kutanikoni; na ijapokuwa hayo yote, mwanamke huyo anajitiisha kwa kupenda chini ya mamlaka ya mwanamume huyo. Katika visa fulani, huenda ikawa mwanamke huyo ni Mkristo mtiwa-mafuta ambaye baadaye atakuwa mmoja wa warithi pamoja na Kristo. Mwanamke huyo atakuwa na cheo cha juu kuliko malaika, atatawala pamoja na Kristo mbinguni. Huo ni mfano mzuri kama nini ambao malaika wanaweza kujionea kwa sasa! Kwa kweli, akina dada wote wana pendeleo zuri kama nini la kuonyesha utii na unyenyekevu kupitia mwenendo wao wa ushikamanifu huku wakitazamwa na mamilioni ya malaika waaminifu!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki