-
Fadhili—Sifa Muhimu Machoni pa MunguMnara wa Mlinzi—2012 | Septemba 1
-
-
Pia, tunakumbushwa hivi: “Msisahau ukaribishaji-wageni,” au kuwatendea kwa fadhili watu tusiowajua.—Waebrania 13:2.
-
-
Fadhili—Sifa Muhimu Machoni pa MunguMnara wa Mlinzi—2012 | Septemba 1
-
-
Inapendeza kuona kwamba baada ya mtume Paulo kuzungumza kuhusu kuwatendea kwa fadhili watu tusiowajua, aliongezea hivi: “Kupitia huo [ukaribishaji-wageni] watu wengine, bila wao wenyewe kujua, waliwakaribisha malaika.” Unaweza kuwazia jinsi ambavyo ungehisi ikiwa ungepewa nafasi ya kuwakaribisha malaika? Lakini kwanza Paulo anasema “bila wao wenyewe kujua.” Kwa maneno mengine, alimaanisha kwamba ikiwa tuna zoea la kuwatendea wengine kwa fadhili, kutia ndani watu tusiowajua kabisa, au hata watu ambao hatuwajui vizuri, huenda tukathawabishwa kwa njia tusizotazamia.
Tafsiri nyingi za Biblia zenye marejezo zinahusianisha maneno ya Paulo na masimulizi kuhusu Abrahamu na Loti yaliyo katika Mwanzo sura ya 18 na 19. Katika visa vyote viwili, tunasoma kuhusu malaika wakiwatokea wakiwa na ujumbe muhimu bila wanaume hao kuwatambua. Katika kisa cha Abrahamu, ujumbe ulihusu utimizo wa ahadi ya Mungu ya kumpa mwana, na katika kisa cha Loti, ujumbe ulihusu kukombolewa kutoka kwa uharibifu uliokuwa ukija juu ya majiji ya Sodoma na Gomora.—Mwanzo 18:1-10; 19:1-3, 15-17.
Ukisoma maandiko yaliyotajwa hapo juu, utaona kwamba Abrahamu na Loti waliwatendea kwa fadhili wapita-njia ambao hawakuwafahamu. Bila shaka, katika nyakati za Biblia, ilikuwa wajibu na pia desturi kwa watu kuwakaribisha wasafiri na wapita-njia, iwe walikuwa marafiki, watu wa ukoo, au watu wasiojulikana. Hata Sheria ya Musa iliwaagiza Waisraeli wasipuuze mahitaji ya watu wasio Waisraeli katika nchi yao. (Kumbukumbu la Torati 10:17-19) Ingawa watu walikuwa na mazoea hayo, inaonekana kwamba Abrahamu na Loti walifanya mengi zaidi kuliko mambo yaliyokuja kuandikwa kwenye sheria baadaye. Walijitahidi isivyo kawaida kuwatendea kwa fadhili watu wasiowajua, na walibarikiwa kwa kufanya hivyo.
Matendo ya Abrahamu ya kuonyesha fadhili hayakumletea yeye mwenyewe tu baraka kwa vile alipata mwana, bali yalitufaidi sisi pia. Kwa njia gani? Abrahamu na mwanaye Isaka walitimiza sehemu muhimu sana katika utimizo wa kusudi la Mungu. Wakawa watu muhimu sana katika ukoo wa familia iliyotokeza yule Masihi, Yesu. Na maisha yao ya uaminifu yalionyesha kimbele jinsi ambavyo Mungu angeweka msingi wa kuwakomboa wanadamu kupitia upendo na fadhili zake zisizostahiliwa.—Mwanzo 22:1-18; Mathayo 1:1, 2; Yohana 3:16.
-