-
Jinsi Ulivyo Kiumbe cha Kipekee!Je, Kuna Muumba Anayekujali?
-
-
[Sanduku katika ukurasa wa 59]
Lugha na Akili
Kwa nini akili ya binadamu inashinda sana akili ya wanyama, kama vile nyani? Jambo kubwa ni uwezo wetu wa kuunganisha sauti kufanyiza maneno na kutumia maneno kufanyiza sentensi. Mtaalamu wa utendaji wa ubongo Dakt. William H. Calvin aeleza:
“Sokwe wasiofugwa hutoa karibu dazani tatu za sauti tofauti-tofauti ili kuwasilisha karibu dazani tatu za maana tofauti-tofauti. Wao waweza kurudia sauti ili kukazia maana, lakini wao hawaunganishi sauti tatu tofauti-tofauti ili kufanyiza neno jipya katika msamiati wao.
“Sisi wanadamu pia hutumia karibu dazani tatu za sauti, ambazo huitwa fonimi. Lakini ni miunganisho ya hizo ndiyo hutokeza maana: sisi huunganisha sauti zisizo na maana ili kuunda maneno yenye maana.” Dakt. Calvin alitaja kwamba “hakuna mtu ambaye ameeleza sababu ya kuwako kwa” tofauti kubwa sana kati ya “sauti moja/maana moja” ya wanyama na uwezo mkubwa wa ajabu wa mwanadamu wa kuunda maneno.
-
-
Jinsi Ulivyo Kiumbe cha Kipekee!Je, Kuna Muumba Anayekujali?
-
-
[Sanduku katika ukurasa wa 60]
Unaweza Kufanya Mengi Kuliko Kuchora Tu Vitu Visivyo na Maana
“Je, ni mwanadamu tu ambaye ana uwezo wa kuwasiliana kwa lugha? Kwa wazi ni lazima jibu litegemee kile kinachomaanishwa na ‘lugha’—kwa kuwa wanyama huwasiliana kwa njia nyingi tofauti-tofauti kama vile ishara, harufu, miito, milio na nyimbo, na hata kucheza dansi kama vile nyuki. Lakini inaonekana kwamba mbali na mwanadamu, wanyama hawana lugha yenye kufuata sarufi. Na jambo muhimu zaidi ni kwamba wanyama hawachori picha za kuwakilisha mambo wanayotaka kuwasilisha. Hawawezi kufanya chochote zaidi ya kuchora tu vitu visivyo na maana.”—Profesa R. S. na D. H. Fouts.
-