-
Viumbe wa Ajabu Katika Pori la TasmaniaAmkeni!—2012 | Aprili
-
-
WAKATI wa mchana, kimya na utulivu hutanda katika pori la Tasmania. Lakini usiku, mingurumo na kelele zenye kuogopesha husikika msituni. Kelele hizo hutoka wapi? Zinatokezwa na mnyama aliye na mbeleko na jina lenye kushangaza—ibilisi wa Tasmania (Tasmanian devil). Wanyama hao wenye nguvu wana sura yenye kuogopesha na sauti yenye kutisha, hasa wanapokula mzoga. Lakini kwa kweli wao si wanyama wenye kutisha.
Wanyama hao wanaweza kumaliza mizoga katika msitu upesi sana. Taya na meno yao yenye nguvu yanaweza kutafuna kila sehemu ya mzoga—ngozi, mifupa, na kila kitu. Kwa kweli, mnyama huyo anaweza kula chakula kinacholingana na asilimia 40 ya uzito wa mwili wake katika muda wa dakika 30, na hiyo ni sawa na mwanadamu kula nyama yenye uzito wa kilo 25 mara moja!
-
-
Viumbe wa Ajabu Katika Pori la TasmaniaAmkeni!—2012 | Aprili
-
-
[Picha katika ukurasa wa 10]
Ibilisi wa Tasmania
[Hisani]
© J & C Sohns/age fotostock
-