-
Kwa Nini Ninahangaikia Sana Uzito Wangu?Amkeni!—1999 | Aprili 22
-
-
“Kuna pambano kali akilini mwangu. Ninapotaka kula, wazo jingine hunijia la kutokula kwa sababu ninahofu kwamba nitaongeza uzito mwingi zaidi.”—Jaimee.
NI NINI unachohofu zaidi ya kitu kingine cho chote? Bila kusita, wasichana wengi watajibu: kuongeza uzito. Kwa hakika, uchunguzi mmoja ulionyesha kwamba wanawake vijana leo huhofu zaidi kuongeza uzito kuliko vita ya nyuklia, kansa, au hata kuwapoteza wazazi wao!
Kwa kushangaza, nyakati nyingine kuhangaikia uzito huanza katika umri mchanga zaidi. Hata kabla ya utineja, wasichana wengi hukutana ili kuwa na “mazungumzo juu ya uzito”—mazungumzo yanayofunua jinsi ambavyo wanachukia miili yao, asema Dakt. Catherine Steiner-Adair. Kwa msingi wa uthibitisho uliopo, ni zaidi ya mazungumzo ya kivivi hivi tu. Katika uchunguzi wa wasichana 2,379, asilimia 40 walikuwa kwa hakika wakijaribu kupunguza uzito. Wale waliohojiwa walikuwa wenye umri wa miaka tisa na kumi tu!
Baada ya muda, huenda wengi wa vijana hawa wakaanza kula milo ya kimtindo. Na lililo baya zaidi ni kwamba huenda baadhi yao watakuwa kama Jenna mwenye umri wa miaka 20. Akiwa na kimo cha futi tano na inchi nne, mwanamke huyu kijana ana uzito wa kilo 40 tu! “Mimi sitaki kula tu,” asema Jenna. “Hangaiko langu kubwa ni kwamba nilitumia muda wa miaka mitatu kupoteza uzito, na kwa kula nitaurudisha katika kipindi cha mwezi mmoja.”
Labda unaweza kuelewa hisia za Jenna. Huenda ikawa kwamba hata wewe umekuwa ukitaka kuwa mwembamba ili uonekane bora zaidi. Kwa hakika, si kosa kuhangaikia sura yako. Hata hivyo, tamaa ya Jenna ya kuwa mwembamba karibu imuue. Jinsi gani?
Kufa Njaa
Jenna anakabiliana na ugonjwa wa ulaji hatari sana wa kukosa hamu ya chakula. Na ndivyo na Jaimee, aliyetajwa mwanzoni. Kwa wakati fulani, wasichana hawa walikuwa wakifa njaa, na ndivyo na wengine. Inakadiriwa kwamba msichana 1 kati ya 100 ana ugonjwa wa kukosa hamu ya chakula. Hilo lamaanisha kwamba mamilioni ya wanawake vijana wameathiriwa—labda hata mtu fulani umjuaye!a
Ugonjwa wa kukosa hamu ya chakula waweza kuibuka kwa njia rahisi sana. Msichana mdogo aweza kuamua kula mlo usioonekana kuwa na madhara, ili labda apoteze kilo chache tu. Hata hivyo, anakosa kuridhika afikiapo mradi wake. “Mimi bado ni mnene sana!” yeye asema anapojitazama bila furaha kwenye kioo. Hivyo anaamua kupunguza kilo chache zaidi. Kisha kilo nyingine chache. Na nyingine zaidi. Linakuwa zoea, na ugonjwa wa kukosa hamu ya chakula unaanza kusitawi.
Bila shaka, si wote wenye kujinyima chakula walio na ugonjwa wa kukosa hamu ya chakula. Wengine wana hangaiko halali la uzito wao, na kwa watu hawa, kupunguza kilo chache kwaweza kuwa na manufaa. Lakini wasichana wengi wana maoni yaliyopotoka juu ya mwili wao. Gazeti la FDA Consumer hulinganisha kuwa na umbo baya la mwili na kujitazama katika kioo kinachopotosha kuonekana kwa umbo la mwili. “Unajiona ukiwa mnene kuliko ulivyo,” gazeti hilo lasema.
Kwa sababu hiyo, mtu aliye na ugonjwa wa kukosa hamu ya chakula huwa na hofu isiyofaa ya kuongeza uzito—hata ajapokuwa mwembamba kama kijiti. Huenda akafanya mazoezi kwa bidii ili abaki akiwa mwembamba na kujipima uzito mara kadhaa kwa siku ili kuhakikisha kwamba harudishi uzito aliopunguza. Anaweza kula chakula kidogo sana. Au huenda asile kabisa. “Kila siku ningeenda shuleni na chakula cha mchana alichonitayarishia mama, na karibu kila siku ningetupa chakula hicho,” asema Heather. “Punde si punde nikazoea kutokula hivi kwamba hata nilipotaka kula, nilishindwa. Sikuhisi njaa.”
Mwanzoni, watu wenye ugonjwa wa kukosa hamu ya chakula kama Heather hufurahi sana wanapopunguza uzito. Lakini hatimaye ukosefu wa lishe inayofaa huanza kuwaathiri. Mtu mwenye kukosa hamu ya chakula huwa mchovu na mwenye kusinzia. Kazi yake ya shule huanza kuathiriwa. Huenda akakosa hedhi.b Baada ya muda, huenda mpigo wa moyo na msongo wa damu ukashuka sana. Na bado, mtu mwenye kukosa hamu ya chakula huwa hatambui hatari yoyote. Kwa hakika, hatari moja tu anayoona ni kurudisha uzito aliopunguza—hata kilo moja tu ya uzito huo.
-
-
Kwa Nini Ninahangaikia Sana Uzito Wangu?Amkeni!—1999 | Aprili 22
-
-
Hatari za Kiafya
Matatizo yote matatu ya ulaji yanaweza kuhatarisha sana afya ya mtu. Kukosa hamu ya chakula kwaweza kusababisha utapiamlo mbaya sana, na katika visa vingi—wengine hukadiria kwamba asilimia 15 ya visa—huweza kusababisha kifo. Kula kupita kiasi, kuwe kunafuatwa na usafishaji wa tumbo au la, ni hatari kwa afya. Baada ya muda, kunenepa sana kwaweza kutokeza maradhi ya mishipa ya moyo yaliyo hatari kwa uhai, kisukari, na hata aina fulani za kansa. Kujilazimisha kutapika kwaweza kuharibu umio, na matumizi ya kupita kiasi ya dawa za kuharisha na kukojoza yaweza katika visa vibaya zaidi kusababisha shtuko la moyo.
Hata hivyo, kuna jambo jingine kuhusu matatizo ya ulaji linalohitaji kufikiriwa. Kwa kawaida wale walio na tatizo la kukosa hamu ya chakula, kuwa na hamu ya chakula isiyo ya kawaida, na kula kusikodhibitiwa hukosa furaha. Wao huelekea kukosa kujistahi, kuwa na mahangaiko na kuwa na mshuko-moyo. Kwa wazi, wanahitaji msaada. Lakini wale walio na tatizo la ulaji wanaweza kusaidiwaje kuepuka kuhangaikia sana uzito? Swali hili litazungumziwa katika makala ya wakati ujao katika mfululizo huu.
-