-
Mpinga-KristoKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Je, Biblia inasema kwamba kuna mpinga-Kristo mmoja tu?
1 Yoh. 2:18: “Watoto wachanga, ni saa ya mwisho, na, kama vile ambavyo mmesikia kwamba mpinga-Kristo anakuja, hata sasa kumekuwa na wapinga-Kristo wengi; uhakika ambao kutokana nao tunajua kwamba ni saa ya mwisho.”
2 Yoh. 7: “Wadanganyifu wengi wametokea katika ulimwengu, watu ambao hawamkiri Yesu Kristo kuwa alikuja katika mwili. Hao ndio yule mdanganyifu na mpinga-Kristo.” (Ona kwamba “wapinga-Kristo wengi” katika 1 Yohana 2:18 wanatajwa hapa kwa ujumla kuwa ndiye “mpinga-Kristo.”)
-
-
Mpinga-KristoKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Baadhi ya wale wanaotambulishwa kuwa mpinga-Kristo—
Watu wanaokana kwamba kwa kweli Yesu ndiye Masihi
1 Yoh. 2:22: “Ni nani aliye mwongo kama si yule anayekana kwamba Yesu ndiye Kristo [au, Masihi, mtiwa-mafuta]? Huyo ndiye mpinga-Kristo.”
Wote wanaokana kwamba Yesu ndiye Mwana wa pekee wa Mungu
1 Yoh. 2:22: “Huyo ndiye mpinga-Kristo, yeye anayemkana Baba na Mwana.”
Linganisha na Yohana 10:36; Luka 9:35.
Waasi-imani
1 Yoh. 2:18, 19: “Kumekuwa na wapinga-Kristo wengi . . . Wao waliondoka kwetu, lakini hawakuwa wa namna yetu.”
Wale wanaowapinga wafuasi wa kweli wa Kristo
Yoh. 15:20, 21: “Ikiwa wamenitesa mimi, watawatesa ninyi pia . . . Lakini watawatendea mambo yote haya kwa ajili ya jina langu.”
Watu mmoja-mmoja na mataifa yanayompinga Kristo akiwa Mfalme au ambayo yanadai kwa uwongo kuwa na cheo cha Kimasihi
Zab. 2:2: “Wafalme wa dunia wanachukua msimamo wao nao maofisa wakuu wamejikusanya pamoja kama mtu mmoja dhidi ya Yehova na dhidi ya mtiwa-mafuta [Kristo, au Masihi] wake.”
Ona pia Ufunuo 17:3, 12-14; 19:11-21.
Mt. 24:24: “Makristo wa uwongo na manabii wa uwongo watatokea na kutoa ishara kubwa na maajabu ili kuwapotosha, ikiwezekana, hata wale waliochaguliwa.”
-