-
Kwa Nini Tumtambue Mpinga-Kristo?Mnara wa Mlinzi—2006 | Desemba 1
-
-
Mtume Yohana ndiye mwandikaji pekee wa Biblia ambaye anatumia neno “mpinga-Kristo.” Katika barua mbili zinazoitwa kwa jina lake, neno hilo linaonekana mara tano likiwa kwa umoja au kwa wingi. Mistari yenye neno hilo inaonyeshwa katika sanduku kwenye ukurasa unaofuata.
-
-
Mpinga-Kristo AnafunuliwaMnara wa Mlinzi—2006 | Desemba 1
-
-
[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 4]
KILE AMBACHO BIBLIA INASEMA KUHUSU MPINGA-KRISTO
“Watoto wachanga, ni saa ya mwisho [kwa wazi, mwisho wa siku za mitume], na, kama vile ambavyo mmesikia kwamba mpinga-Kristo anakuja, hata sasa kumekuwa na wapinga-Kristo wengi.” —1 Yohana 2:18.
“Ni nani aliye mwongo kama si yule anayekana kwamba Yesu ndiye Kristo? Huyo ndiye mpinga-Kristo, yeye anayemkana Baba na Mwana.”—1 Yohana 2:22.
“Kila neno lililoongozwa na roho ambalo halimkiri Yesu halitokani na Mungu. Zaidi ya hayo, hili ndilo neno lililoongozwa na roho la yule mpinga-Kristo ambalo mmesikia kwamba linakuja, na sasa tayari limo ulimwenguni.” —1 Yohana 4:3.
“Kwa maana wadanganyifu wengi wametokea katika ulimwengu, watu ambao hawamkiri Yesu Kristo kuwa alikuja katika mwili. Hao ndio yule mdanganyifu na mpinga-Kristo.”—2 Yohana 7.
-