Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Mababa wa Kanisa Walikuwa Watetezi wa Kweli ya Biblia?
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Aprili 15
    • Katika pindi hiyo, waandishi na watu wenye kufikiri sana waliohisi kwamba ilikuwa lazima kufasiri mafundisho ya “Kikristo” kwa kutumia semi za kifalsafa walianza kuongezeka. Ili kuridhisha wapagani walioelimika ambao walikuwa wageuzwa-imani wapya wa “Kikristo,” waandishi hao wa kidini walitegemea sana vichapo vya mapema vya Kigiriki na Kiyahudi. Kuanzia na mwandishi Justin Martyr (karibu 100-165 W.K.), aliyeandika kwa Kigiriki, watu waliodai kuwa Wakristo walizidi kuwa wazoefu katika kuchanganya maoni na mafundisho ya wanafalsafa Wagiriki na yale ya Kikristo.

      Mwelekeo huo ulijitokeza sana katika maandishi ya Origen (karibu 185-254 W.K.), aliyekuwa mwandishi Mgiriki wa Alexandria. Simulizi la Origen katika kichapo On First Principles lilikuwa hatua ya kwanza iliyofanywa kwa utaratibu kueleza mafundisho makuu ya theolojia ya “Kikristo” kwa kutumia falsafa ya Kigiriki.

  • Je, Mababa wa Kanisa Walikuwa Watetezi wa Kweli ya Biblia?
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Aprili 15
    • Hivi karibuni, Kasisi wa Othodoksi ya Ugiriki, Methodius wa Pisidia aliandika kitabu The Hellenic Pedestal of Christianity ili kuonyesha kwamba utamaduni na falsafa ya Kigiriki ndio msingi wa “Ukristo” wa leo. Katika kitabu hicho, akiri hivi pasipo kusita: ‘Karibu Mababa wote wa Kanisa waliona falsafa za Kigiriki cha kale kuwa muhimu sana, na kuzitumia ili kuelewa na kufafanua kwa usahihi kweli za Kikristo.’

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki