Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kushikilia kwa Imara Jina la Yesu
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 14. (a) Tangu siku za mapema, kundi la Kikristo limelazimika kushindana na akina nani, na mtume Paulo aliwaelezaje? (b) Ni maneno gani ya Yesu yanayopasa kutiiwa na yeyote ambaye huenda ikawa ameelekea kufuata kikundi chenye kujitenga mbali?

      14 Tangu siku za mapema, kundi la Kikristo limekuwa halina budi kushindana na waasi-imani wenye kiburi, ambao kwa usemi laini, wenye kudanganya “husababisha migawanyiko na sababu za kukwaza kinyume cha fundisho” lililoandaliwa kupitia mfereji wa Yehova. (Waroma 16:17, 18, NW) Mtume Paulo alionya juu ya tisho hili karibu katika barua zake zote.a Katika nyakati za ki-siku-hizi, wakati ambapo Yesu amerudishia kundi la Kikristo la kweli usafi na umoja walo, hatari ya farakano inabaki. Kwa sababu hiyo, yeyote ambaye huenda alikuwa ameelekea kufuata kikundi chenye kujitenga mbali, hivyo kufanyiza farakano, apaswa atii maneno yafuatayo ya Yesu: “Kwa hiyo tubu. Usipofanya hivyo, mimi naja kwako upesi, nami nitapiga vita nao kwa upanga mrefu wa kinywa changu.”—Ufunuo 2:16, NW.

      15. Farakano linaanzishwaje?

      15 Farakano linaanzishwaje? Pengine mwalimu fulani wa kujifanya anapanda mashaka, akibishia ukweli fulani wa Biblia (Kama vile kuwa kwetu sisi katika siku za mwisho), na hivyo kikundi kilicho kisehemu kinavunjika na kutoka kumfuata yeye. (2 Timotheo 3:1; 2 Petro 3:3, 4) Au mtu fulani anachambua ile njia ambayo katika hiyo Yehova anafanyiza kazi yake naye anavuta ile roho ya kutofanya mengi sana kwa kudai kwamba kwenda nyumba kwa nyumba na ujumbe wa Ufalme si njia ya Kimaandiko wala haihitajiwi kabisa. Kushiriki utumishi kama huo kufuatia kielelezo cha Yesu na mitume wake kungewaendeleza hawa wakiwa wanyenyekevu; hata hivyo, wao wanaona ni afadhali wajitenge na kujistarehesha, pengine wakisoma Biblia tu pindi kwa pindi wakiwa kikundi cha faragha. (Mathayo 10:7, 11-13; Matendo 5:42; 20:20, 21) Watu kama hao wanabuni mawazo yao wenyewe juu ya Ukumbusho wa Kifo cha Yesu, ile amri ya Kimaandiko ya kuepukana na damu, kusherehekea sikukuu, na tumizi la tumbako. Zaidi ya hilo, wao wanashushia heshima jina la Yehova; upesi sana wanaanguka na kurudi ndani ya njia zenye kuendekeza za Babuloni Mkubwa. Hata vibaya zaidi, baadhi yao wanasukumwa na Shetani wageukie na ‘kupiga watumwa wenzao,’ ambao wakati mmoja walikuwa ndugu zao.—Mathayo 24:49; Matendo 15:29; Ufunuo 17:5, NW.

  • Kushikilia kwa Imara Jina la Yesu
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • a Ona pia 1 Wakorintho 3:3, 4, 18, 19; 2 Wakorintho 11:13; Wagalatia 4:9; Waefeso 4:14, 15; Wafilipi 3:18, 19; Wakolosai 2:8; 1 Wathesalonike 3:5; 2 Wathesalonike 2:1-3; 1 Timotheo 6:3-5; 2 Timotheo 2:17; 4:3, 4; Tito 1:13, 14; 3:10; Waebrania 10:26, 27.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki