-
“Mimi Ni . . . Mnyenyekevu Moyoni”‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
-
-
Lakini, usiku uliotangulia kifo chake, aliona kwamba ingawa mitume wake walikuwa wakifanya yote wawezayo kuondolea mbali kiburi, bado walikuwa na udhaifu huo. Kisha, akawafundisha somo ambalo hawakusahau. Alijifunga kitambaa kiunoni na kufanya kazi ya hali ya chini zaidi, ambayo watumishi wa siku hizo walikuwa wakiwafanyia wageni. Yesu aliosha miguu ya mitume wake wote, hata Yuda, aliyemsaliti muda mfupi baadaye!—Yohana 13:1-11.
18 Yesu alikazia jambo kuu aliposema: “Niliweka kielelezo kwa ajili yenu.”
-
-
“Mimi Ni . . . Mnyenyekevu Moyoni”‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
-
-
22 Kwa kweli, Petro hakuusahau usiku ambao Yesu aliosha miguu yake, ijapokuwa Petro mwenyewe hakutaka kuoshwa! (Yohana 13:6-10) Petro aliwaandikia hivi Wakristo: “Jifungeni unyenyekevu wa akili kuelekeana ninyi wenyewe.” (1 Petro 5:5) Neno “jifungeni” linadokeza wazo la mtumishi anayejifunga kitambaa kiunoni ili kufanya kazi ya hali ya chini. Neno hilo linaweza kutukumbusha wakati ambapo Yesu alijifunga kitambaa kiunoni kabla ya kupiga magoti ili kuosha miguu ya mitume wake. Ikiwa tunamfuata Yesu, je, kweli kuna mgawo wowote kutoka kwa Mungu tunaoweza kuuona kuwa wa hali ya chini? Watu wote wanapaswa kuona kwamba tuna unyenyekevu moyoni, kana kwamba tumeufunga kiunoni.
-