Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Maponyo Yote ya Kimuujiza Yanatoka kwa Mungu?
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Mei 1
    • Hata hivyo, katika barua hiyohiyo aliyowaandikia Wakorintho, Paulo alisema pia kwamba zawadi za kimuujiza za roho takatifu ya Mungu zingekoma. Alisema hivi: “Kama kuna zawadi za kutoa unabii, zitaondolewa mbali; kama kuna lugha, zitakoma; kama kuna ujuzi, utaondolewa mbali.”—1 Wakorintho 13:8.

      Katika karne ya kwanza, Yesu Kristo na mitume wake waliwaponya watu kimuujiza. Katika siku za mitume, zawadi za roho kama vile kuwaponya watu, zilikusudiwa kumletea Mungu utukufu na kuonyesha kwamba Yehova alilikubali na kulibariki kutaniko la Kikristo lililokuwa limeanzishwa wakati huo. Lakini baada ya kutaniko la Kikristo kukomaa na kuimarika zawadi za pekee hazikukaziwa sana, bali sifa kama vile imani thabiti, tumaini, na upendo ndizo zilizothibitisha kwamba Wakristo walikubaliwa na Mungu. (Yohana 13:35; 1 Wakorintho 13:13) Kwa hiyo, mwaka wa 100 W.K. hivi, Mungu hakuwapa tena watu uwezo wa kuponya kimuujiza ili kuonyesha kwamba aliwakubali.a

  • Je, Maponyo Yote ya Kimuujiza Yanatoka kwa Mungu?
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Mei 1
    • a Yaelekea mitume walipokufa, hakuna aliyeweza kupitisha zawadi za roho, nazo zilikoma kabisa wakati ambapo wale wote waliokuwa wamepata zawadi hizo walikufa.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki