-
‘Yesu Aliwapenda Mpaka Mwisho’‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
-
-
5 Baadaye, usiku huohuo, Yesu alipoenda katika bustani ya Gethsemane pamoja na wale mitume waaminifu 11, subira yake ilijaribiwa tena. Akiwaacha mitume wake wanane, Yesu aliwachukua Petro, Yakobo, na Yohana na kuingia nao ndani zaidi katika bustani hiyo. Ndipo Yesu akawaambia: “Nafsi yangu ina huzuni sana, kiasi cha kufa. Kaeni hapa na mwendelee kukesha pamoja nami.” Akasonga mbele kidogo, na kuanza kusali kwa bidii. Baada ya kusali kwa muda mrefu, akarudi mahali walipokuwa wale mitume watatu. Aliwakuta wakifanya nini? Saa hiyo, saa aliyokuwa akijaribiwa vikali zaidi, walikuwa wamelala fofofo! Je, aliwakemea kwa sababu hawakukesha? Hapana, aliwahimiza kwa subira. Maneno yake yenye fadhili yalionyesha kwamba alielewa uchovu waliokuwa nao na udhaifu wao mbalimbali.a Alisema: “Bila shaka, roho inataka, lakini mwili ni dhaifu.” Yesu aliendelea kuwa mwenye subira jioni hiyo hata aliporudi na kuwakuta wakiwa wamelala, si mara ya kwanza tu bali pia mara ya pili na ya tatu!—Mathayo 26:36-46.
-
-
‘Yesu Aliwapenda Mpaka Mwisho’‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
-
-
a Mbali na uchovu wa kimwili, kuna jambo lingine lililofanya mitume hao walale. Masimulizi kama hayo kwenye Luka 22:45 yanasema kwamba Yesu ‘aliwakuta wakisinzia kwa huzuni.’
-