Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Wakati wa Kutahini (1914-1918)
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • “Nyakati za Mataifa zimekwisha; siku za wafalme wao zimekwisha”! Ndivyo Ndugu Russell alivyopaaza sauti alipokuwa akiingia chumba cha kulia kwenye makao makuu ya Brooklyn ya Watch Tower Society, asubuhi ya Ijumaa, Oktoba 2, 1914.

  • Wakati wa Kutahini (1914-1918)
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Oktoba 1914 ukapita, na C. T. Russell na washirika wake walikuwa wangali duniani. Kisha Oktoba 1915 ukapita. Je, Russell alikatishwa tamaa? Katika The Watch Tower la Februari 1, 1916, yeye aliandika hivi: “‘Lakini, Ndugu Russell, wazo lako ni nini kuhusu wakati wa kubadilika kwetu? Je, wewe hukukatishwa tamaa kwamba huo hukuja tulipoutazamia kwamba ungekuja?’ mtauliza. Hapana, twajibu, sisi hatukukatishwa tamaa. . . . Ndugu, wale miongoni mwetu walio na maoni yafaayo kuelekea Mungu hawakatishwi tamaa na mipango yoyote Yake. Sisi hatukutaka mapenzi yetu wenyewe yafanyike; hivyo wakati tulipopata kujua kwamba tulikuwa tukitarajia jambo lenye kosa katika Oktoba, 1914, basi tulifurahi kwamba Bwana hakubadili Mpango Wake utufae sisi. Sisi hatukutaka Yeye afanye hivyo. Sisi twataka tu tuweze kuelewa mipango na makusudi Yake.”

  • Wakati wa Kutahini (1914-1918)
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Kama vile The Watch Tower la Septemba 1, 1916, lilivyoeleza jambo hilo: “Sisi tuliwazia kwamba kazi ya Mavuno ya kukusanya kuleta ndani Kanisa [la watiwa-mafuta] ingekamilishwa kabla ya mwisho wa Nyakati za Mataifa; lakini hamkuwa na lolote katika Biblia lililosema hivyo. . . . Je, sisi twasikitika kwa sababu kazi ya Mavuno yaendelea? Hapana, hakika . . . Maoni yetu ya sasa, ndugu wapendwa, yapasa kuwa ya shukrani nyingi kuelekea Mungu, uthamini wenye kuongezeka wa Kweli nzuri ajabu ambayo Yeye ametujalia pendeleo la kuiona na kuhusianishwa nayo, na bidii yenye kuongezeka katika kupeleka Kweli hiyo kwa wengine waijue.”

      Lakini je, kulikuwa mengi zaidi ya kufanywa katika kazi ya mavuno? Kwa wazi Ndugu Russell alifikiri hivyo. Yenye kuonyesha hivyo ni mazungumzo aliyokuwa nayo pamoja na Ndugu Macmillan katika vuli ya 1916. Akimwita Macmillan kwenye ofisi yake alimofanyia funzo na uandishi wake kwenye Betheli ya Brooklyn, Russell alimwambia hivi: “Kazi inaongezeka haraka, na itaendelea kuongezeka, kwa kuwa kuna kazi ya ulimwenguni pote ya kufanywa katika kuhubiri ‘gospeli ya ufalme’ katika ulimwengu wote.” Russell alitumia muda wa saa tatu na nusu akieleza Macmillan kwa ufupi yale aliyoelewa kutoka Biblia kuwa ndiyo kazi kubwa iliyokuwa ingali mbele.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki