Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kukua Katika Ujuzi Sahihi Juu ya Kweli
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Muda mfupi baada ya hapo, katika makala moja yenye kichwa “Nyakati za Mataifa: Zakoma Wakati Gani?,” Russell pia alitoa sababu juu ya habari hiyo kwa kutumia Maandiko akataarifu kwamba uthibitisho ulionyesha kwamba “nyakati saba zitakoma katika A.D. 1914.” Makala hiyo ilichapwa katika toleo la Oktoba 1876 la Bible Examiner.j Kile kitabu Three Worlds, and the Harvest of This World, kilichotokezwa katika 1877 na N. H. Barbour kwa kushirikiana na C. T. Russell, kilielekeza kwenye mkataa huohuo. Baada ya hapo, matoleo ya mapema ya Watch Tower, kama yale ya tarehe ya Desemba 1879 na Julai 1880, yalivuta fikira kwenye 1914 W.K. kuwa mwaka wa maana sana kwa maoni ya unabii wa Biblia. Katika 1889 sura nzima ya nne ya Buku 2 la Millennial Dawn (baadaye liliitwa Studies in the Scriptures) ilitumiwa kuzungumzia “Nyakati za Mataifa.”

  • Kukua Katika Ujuzi Sahihi Juu ya Kweli
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • The Watch Tower la Februari 1, 1916, lilivuta fikira hususa kwenye Oktoba 1, 1914, kisha likasema: “Hiyo ilikuwa ndiyo hatua ya mwisho ya wakati ambayo kronolojia ya Biblia ilielekeza kwetu kuwa ilihusiana na mambo ambayo yangelipata Kanisa la Katoliki ya Roma. Je, Bwana alituambia kwamba tungechukuliwa huko [mbinguni]? Hapana. Yeye alisema nini? Neno lake na matimizo ya unabii yalionekana yakielekeza bila kukosea kwamba tarehe hiyo ilionyesha mwisho wa Nyakati za Mataifa. Sisi tuliamua kutokana na hilo kwamba ‘badiliko’ la Kanisa lingetukia katika au kabla ya tarehe hiyo. Lakini Mungu hakutuambia kwamba ingekuwa hivyo. Yeye alituruhusu tufikie uamuzi huo; nasi tunaamini kwamba umethibitika kuwa mtihani uliohitajiwa juu ya watakatifu wapendwa wa Mungu kila mahali.” Lakini je, matukio hayo yalithibitisha kwamba tumaini lao tukufu lilikuwa limekuwa la bure? Hapana. Ilimaanisha tu kwamba si kila kitu kilikuwa kikitukia upesi kama walivyokuwa wametarajia.

      Miaka kadhaa kabla ya 1914, Russell alikuwa ameandika hivi: “Kwa wazi kronolojia (unabii wa wakati kwa ujumla) haikukusudiwa kuwapa watu wa Mungu habari sahihi ya kronolojia muda wa karne zote. Kwa wazi ilikusudiwa zaidi itumike kama kengele ya saa iwaamshe na kuwatia nishati watu wa Bwana katika wakati ufaao. . . . Lakini tuseme, mathalani, kwamba Oktoba, 1914, ungepita na kusitukie anguko kubwa la serikali za Mataifa. Hilo lingethibitisha au lisingethibitisha nini? Lisingeondoa uthibitisho wa sehemu yoyote ya Mpango wa Kimungu wa Zile Enzi. Bei ya fidia iliyokamilishwa huko Kalvari bado ingekuwa uthibitisho wa utimizo wa mwisho wa Programu ya Kimungu iliyo kubwa kwa ajili ya rudisho la wanadamu. Ule ‘mwito wa juu’ wa Kanisa lipate kuteseka pamoja na Mkombozi na kutukuzwa pamoja naye likiwa washiriki wake au likiwa Bibi-Arusi wake bado ungekuwa vile vile. . . . Jambo pekee lililoathiriwa na kronolojia lingekuwa wakati wa kutimizwa kwa matumaini hayo matukufu kwa ajili ya Kanisa na kwa ajili ya ulimwengu. . . . Na tarehe hiyo ikipita ingethibitisha tu kwamba kronolojia yetu, ‘kengele ya saa’ yetu, ililia mapema kidogo kabla ya wakati. Je, sisi tungefikiri kwamba ni msiba mkuu ikiwa kengele ya saa yetu ingetuamsha nukta chache mapema zaidi asubuhi ya siku fulani kuu yenye kujawa na shangwe na furaha? Hakika sivyo!”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki