-
Kristo Analiongoza Kutaniko LakeMnara wa Mlinzi—2002 | Machi 15
-
-
Kiongozi wetu hutumia Baraza hilo Linaloongoza kuweka rasmi wanaume wanaostahili—wawe watiwa-mafuta kwa roho au la—kuwa wazee katika makutaniko ya kwao. Kuhusiana na hilo, roho takatifu, ambayo Yehova amempa Yesu mamlaka ya kuitumia, inatimiza jukumu muhimu sana. (Matendo 2:32, 33) Kwanza kabisa, lazima waangalizi hao watimize matakwa yanayoonyeshwa katika Neno la Mungu lililopuliziwa kwa roho takatifu. (1 Timotheo 3:1-7; Tito 1:5-9; 2 Petro 1:20, 21) Kupendekezwa na kuwekwa rasmi hufanywa baada ya sala na chini ya uongozi wa roho takatifu. Isitoshe, watu waliowekwa rasmi wanadhihirisha matunda ya roho hiyo. (Wagalatia 5:22, 23) Hivyo, ushauri huu wa Paulo unawahusu wazee wote, wawe watiwa-mafuta au la: “Kazieni uangalifu kwa nyinyi wenyewe na kundi lote, ambalo miongoni mwalo roho takatifu imewaweka nyinyi rasmi kuwa waangalizi.” (Matendo 20:28)
-
-
Kristo Analiongoza Kutaniko LakeMnara wa Mlinzi—2002 | Machi 15
-
-
Bila shaka, kuishi kulingana na wakfu na ubatizo wetu kunamaanisha kwamba tunatambua uhalali wa mamlaka yaliyowekwa rasmi kutanikoni kupitia roho, na tunakuwa tayari kujitiisha kwa mamlaka hayo. Ubatizo wetu ‘katika jina la roho takatifu’ ni tangazo la hadharani kwamba tunatambua roho takatifu na kukubali jukumu inayotimiza katika makusudi ya Yehova. (Mathayo 28:19) Ubatizo huo unamaanisha kwamba tunashirikiana na roho na tunaepuka kufanya chochote kinachoweza kuzuia roho hiyo isitende kazi miongoni mwa wafuasi wa Kristo. Kwa kuwa roho takatifu inatimiza jukumu muhimu katika kupendekezwa na kuwekwa rasmi kwa wazee, hatuwezi kuwa waaminifu kwa wakfu wetu ikiwa hatuungi mkono mpango wa kuwa na wazee kutanikoni.
-