-
Kwa Nini Tukutanike Pamoja?Mnara wa Mlinzi—2007 | Mei 15
-
-
Kwa Nini Tukutanike Pamoja?
MUME wa Christine alimwacha ghafula baada ya kuishi naye kwa miaka 20 katika ndoa. Christine alijikuta peke yake na kulazimika kuwalea wana saba na binti mmoja. Umri wa watoto hao ulikuwa kati ya miaka 7 na 18. “Sasa ilinibidi kufanya maamuzi yote mazito nikiwa peke yangu,” anasema. “Nilihisi nimelemewa na daraka hilo na nikatamani kupata utegemezo na mwongozo.” Alipata wapi msaada aliohitaji?
“Mikutano ya Kikristo iliniokoa mimi na familia yangu,” Christine anasema. “Katika mikutano, tulipata utegemezo wa marafiki wetu na mwongozo kutoka kwa Neno la Mungu. Kuhudhuria mikutano kwa ukawaida kulitusaidia katika kila jambo muhimu la maisha yetu ya familia.”
-
-
Kwa Nini Tukutanike Pamoja?Mnara wa Mlinzi—2007 | Mei 15
-
-
Fikiria maelezo haya ya mwanamke mmoja Mkristo aliye na ugonjwa wa kudumu. “Kwa sababu ya ugonjwa wangu ninalazimika kukaa hospitalini kwa muda fulani,” anasema. “Kwenda mikutanoni baada ya kukaa hospitalini kwa muda fulani si rahisi, lakini mahali panaponifaa ni katika mikutano. Uchangamfu na upendo wa akina ndugu na dada unachochea shangwe yangu, na mafundisho na mwongozo ambao Yehova na Yesu wanatoa unanifanya niwe na kusudi maishani.”
-