Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ugarit—Jiji la Kale Lililokuwa Kwenye Kitovu cha Ibada ya Baali
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Julai 15
    • Katika maandishi ya Ras Shamra, Baali anaitwa mwana wa Dagani, lakini maana ya neno “mwana” hapa si hakika.

  • Ugarit—Jiji la Kale Lililokuwa Kwenye Kitovu cha Ibada ya Baali
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Julai 15
    • Dini Katika Jiji la Baali

      Zaidi ya miungu ya kiume na ya kike 200 inatajwa katika maandishi ya Ras Shamra. Eli, anayeitwa baba wa miungu na wa wanadamu, ndiye aliyekuwa mungu mkuu kuliko wote. Naye Baali-Hadadi, mungu wa dhoruba, alikuwa “mpanda mawingu” na “bwana wa dunia.” Mungu Eli ni mwanamume mzee mwenye ndevu nyeupe na mwenye hekima, aliye mbali sana na wanadamu. Kwa upande mwingine, Baali ni mungu mwenye nguvu na mwenye kutaka makuu ambaye hutafuta kutawala miungu na wanadamu.

      Maandishi yaliyovumbuliwa huenda yalikuwa yakisomwa wakati wa sikukuu za kidini, kama vile sikukuu za mwaka mpya au za mavuno. Hata hivyo, ufafanuzi sahihi haueleweki. Katika shairi moja kuhusu ugomvi juu ya uongozi, Baali anamshinda mungu wa bahari, Yamm, ambaye ni mwana mpendwa wa mungu Eli. Ushindi huo labda uliwapa mabaharia wa Ugarit uhakika wa kwamba Baali angeweza kuwalinda baharini. Katika mapambano na Moti, Baali anashindwa na kushuka katika ulimwengu wa chini. Hivyo, ukame unatokea na utendaji mbalimbali wa wanadamu unakoma. Mke wa Baali na dada wa Anati—mungu wa kike wa upendo na vita—anamwua Moti na kumrudishia Baali uhai. Baali anawaangamiza wana wa mke wa mungu Eli, Athariti (Ashera), na anachukua tena utawala. Lakini Moti anarudi baada ya miaka saba.

      Watu fulani hueleza shairi hilo kuwa mfano wa mzunguko wa majira mwakani wakati mvua za kutoa uhai zinaposhindwa na joto kali la majira ya joto na kurudi kwa majira ya majani kupukutika. Wengine hufikiri kwamba miaka saba ya mzunguko wa majira inahusiana na woga wa njaa na ukame. Katika hali yoyote ile, ukuu wa Baali ulionekana kuwa muhimu kwa mafanikio ya jitihada za mwanadamu. Mtaalamu Peter Craigie anasema hivi: “Kusudi la dini ya Baali lilikuwa kuhifadhi mamlaka yake; hivyo waabudu wake waliamini kwamba, maadamu tu alibaki mwenye uwezo, mavuno na mifugo ambayo ni muhimu kwa mwanadamu vingeendelea kuhifadhiwa.”

      Ulinzi Dhidi ya Upagani

      Maandishi yaliyovumbuliwa ndani ya udongo yanaonyesha wazi upotovu wa maadili wa dini ya Ugarit. Kitabu The Illustrated Bible Dictionary kinaeleza hivi: “Maandishi hayo yanaonyesha matokeo mapotovu ya kuabudu miungu hiyo nayo yanakazia vita, ukahaba mtakatifu, upendo wa mahaba, na upotovu wa maadili katika jamii unaotokana na mambo hayo.” De Vaux anasema hivi: “Mtu anaposoma mashairi hayo, anaelewa machukizo ambayo waabudu wa kweli wa Yahweh kati ya Waebrania wa kale na manabii wakubwa walihisi kuhusu ibada hiyo.” Sheria ambayo Mungu alilipa taifa la kale la Israeli iliwalinda dhidi ya dini hiyo ya uwongo.

      Mazoea ya uaguzi, kutabiri kwa kutumia nyota, na uchawi, yalienea katika jiji la Ugarit. Dalili na ishara zilitafutwa katika vitu vya mbinguni na pia katika vijusi vyenye kasoro na viungo vya ndani vya wanyama. Mwanahistoria Jacquiline Gachet anaeleza hivi: “Iliaminiwa kwamba mnyama aliyetolewa dhabihu kwa mungu fulani aliungana na mungu huyo na kuwa kitu kimoja, nazo roho zao pia ziliungana. Kwa hiyo, kwa kusoma dalili zinazoonekana juu ya viungo hivyo, iliwezekana kujua mapenzi ya roho ya miungu ambayo ingeweza kutoa jibu nzuri au mbaya kwa swali juu ya matukio ya wakati ujao au juu ya mambo ya kufanya katika hali fulani hasa.” (Le pays d’Ougarit autour de 1200 av.J.C). Tofauti na hilo, Waisraeli walipaswa kuepuka mazoea kama hayo.—Kumbukumbu la Torati 18:9-14.

      Sheria ya Mungu ilikataza waziwazi kulala na mnyama. (Mambo ya Walawi 18:23) Zoea hilo lilionwaje katika jiji la Ugarit? Katika maandishi yaliyovumbuliwa, Baali alionekana akifanya ngono na ndama-jike. “Ikiwa ilisemwa kwamba Baali anachukua umbo la ng’ombe-dume wakati wa tendo hilo,” akaeleza Cyrus Gordon, mtaalamu wa vitu vya kale “makuhani walioigiza tendo hilo hawakuhitaji kuchukua umbo la ng’ombe-dume.”

      Waisraeli waliamriwa hivi: “Musijikate mwili kwa ajili ya wafu.” (Mambo ya Walawi 19:28, ZSB) Hata hivyo, akiomboleza kifo cha Baali, Eli “alikata mwili wake kwa kisu, akajitia alama kwa wembe, akajikata mashavu na kidevu.” Zoea hilo la kujikata-kata lilikuwa jambo la kawaida kati ya waabudu wa Baali.—1 Wafalme 18:28.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki