-
Afrika Kusini2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Katika mwaka wa 2001, jumba lingine pia lilikamilishwa huko Midrand, katikati ya Pretoria na Johannesburg.
Majirani ambao mwanzoni walipinga ujenzi huko Midrand walibadili mtazamo wao walipopata kuwajua akina ndugu na kuona kazi yao. Jirani mmoja alijitolea kuwapelekea matunda na mboga kila baada ya majuma mawili kwa zaidi ya mwaka mmoja. Kampuni kadhaa zilichochewa kutoa michango. Kampuni moja ilitoa mbolea kwa ajili ya bustani bila kutoza chochote. Nyingine iliwapa akina ndugu hundi ya dola za Marekani zipatazo 1,575, kwa ajili ya ujenzi. Bila shaka, akina ndugu pia walitoa michango kwa ukarimu kwa ajili ya ujenzi wa Jumba la Kusanyiko.
Jumba hilo ni maridadi nalo limeundwa vizuri. Guy Pierce, mshiriki wa Baraza Linaloongoza ambaye alitoa hotuba ya wakfu, alizungumzia umaridadi halisi wa jumba hilo, yaani, kumtukuza Mungu wetu Mkuu, Yehova.—1 Fal. 8:27.
-
-
Afrika Kusini2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 150]
Jumba la Kusanyiko la Midrand
-