-
Ninawezaje Kuepuka Kupendezwa na Watu Wasiofaa?Amkeni!—2005 | Agosti 22
-
-
“Nilianza kushirikiana na msichana fulani shuleni. . . . Hakutumia dawa za kulevya, wala kwenda kwenye karamu zisizofaa, naye hakuwa na wapenzi wengi. Hata hakutumia maneno machafu, naye alipata maksi za juu. Lakini kwa kweli hakuwa rafiki anayefaa.”—Beverly.a
KWA nini Beverly alifikia mkataa huo? Sasa anatambua kwamba msichana huyo alimfanya ajihusishe na mazoea yenye kudhuru. Beverly anaeleza: “Nilipoendelea kushirikiana naye, nilianza kusoma vitabu vinavyohusiana na pepo, na hata nikaandika hadithi kuhusu mambo hayo.”
-
-
Ninawezaje Kuepuka Kupendezwa na Watu Wasiofaa?Amkeni!—2005 | Agosti 22
-
-
Kwa kuwa mwanashule wa Beverly hakumwabudu Mungu wa kweli, je, Beverly alipaswa kujihadhari kuhusu kufanya urafiki naye? Kwa kweli, Wakristo wa kweli hawasemi kwamba mtu ana mwenendo usiofaa au ni mwenye maadili mabaya kwa sababu tu yeye si mwamini mwenzao. Lakini mtu anapotaka kuwa na rafiki wa karibu, ni vizuri kuwa mwangalifu. Mtume Paulo aliwaonya hivi watu katika kutaniko la Korintho la karne ya kwanza: “Mashirika mabaya huharibu tabia nzuri.” (1 Wakorintho 15:33) Alimaanisha nini?
Huenda baadhi ya Wakristo hao Wakorintho walikuwa wakishirikiana na Waepikurea waliokuwa wafuasi wa mwanafalsafa Mgiriki Epikurasi. Ni kweli kwamba Epikurasi aliwafundisha wafuasi wake waishi kwa utimamu wa akili, ujasiri, kujizuia, na haki. Hata aliwaonya dhidi ya kufanya makosa ya siri. Kwa hiyo, kwa nini Paulo aliwaona Waepikurea, na wengine katika kutaniko waliokuwa na maoni kama hayo kuwa “mashirika mabaya”?
Waepikurea hawakumwabudu Mungu wa kweli. Kwa kuwa hawakuamini kwamba kuna ufufuo wa wafu, walihangaikia hasa maisha ya sasa na jinsi ambavyo wangepata faida. (Matendo 17:18, 19, 32) Haishangazi kwamba kwa kushirikiana na watu kama hao, wengine katika kutaniko la Korintho walianza kupoteza imani katika ufufuo. Ndiyo sababu katika 1 Wakorintho sura ya 15, ambapo tunapata onyo la Paulo kuhusu mashirika mabaya, kuna maelezo mengi yaliyoandikwa ili kuwasadikisha Wakristo hao wa mapema kuhusu uhalisi wa tumaini la ufufuo.
Tunajifunza nini? Hata watu wasiomwogopa Mungu wanaweza kuwa na sifa nzuri. Lakini ukiwafanya wawe marafiki wa karibu, wataathiri fikira, imani, na mwenendo wako. Kwa hiyo, katika barua yake ya pili kwa Wakorintho, Paulo alisema: “Msifungwe nira isivyo sawa pamoja na wasio waamini.”—2 Wakorintho 6:14-18.
-