Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mtumaini Yehova Upate Mwongozo na Ulinzi
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Nchi Yenye Umwagikaji wa Damu

      3. Fafanua jinsi ambavyo Ashuru ilizingatia sana uwezo wa kijeshi.

      3 Waashuri walijulikana kwa sababu ya uwezo wao wa kijeshi. Kitabu cha Ancient Cities chataarifu hivi: “Waliabudu nguvu, nao wangesali tu kwa sanamu kubwa za mawe, simba na mafahali ambao miguu yao, mabawa yao ya tai, na vichwa vyao vya kibinadamu vyenye nguvu mno vilikuwa ishara ya nguvu, moyo mkuu, na ushindi. Kazi ya taifa hilo ilikuwa vita, na makuhani walichochea vita daima.” Basi yafaa kwamba Nahumu, nabii wa Biblia, alifafanua Ninawi, jiji kuu la Ashuru, kuwa “mji wa damu.”—Nahumu 3:1.

      4. Waashuri walitiaje hofu katika mioyo ya mataifa mengine?

      4 Mbinu za kivita za Waashuri zilikuwa zenye ukatili usio wa kawaida. Mawe yaliyochongwa ya nyakati hizo yaonyesha wapiganaji Waashuri wakitwaa mateka kwa kutumia kulabu zilizotiwa puani au midomoni. Walitumia mikuki kuwapofusha baadhi ya mateka. Mwandiko mmoja wasema kuhusu ushindi fulani ambapo jeshi la Ashuru liliwakata mateka wake vipande-vipande na kujenga vilima viwili nje ya jiji—kimoja cha vichwa na kingine cha miguu na mikono. Watoto wa washinde walichomwa kwa moto. Hapana budi kwamba hofu iliyotokezwa na ukatili huo iliwasaidia Waashuri kijeshi, kwa kuwa iliwavunja moyo wale waliopinga majeshi yao.

  • Mtumaini Yehova Upate Mwongozo na Ulinzi
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • [Picha katika ukurasa wa 209]

      Waashuri walikuwa na kawaida ya kuwapofusha baadhi ya mateka wao

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki